Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

KUELEKEA TAMASHA LA 15 LA JINSIA, TGNP YAJIVUNIA MAFANIKIO YA KAMPENI, SHERIA



Na Avila Kakingo, Michuzi Tv
KUELEKEA tamasha la 15 la jinsia Novemba 7-10, 2023 na Tapo la Ukombozi wa mwanamke Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) unajivunia mafanikio ya baadhi ya sheria kurekebishwa hapa nchini na kampeni mbalimbali kushika hatamu na Kuwa ajenda ya serikali.


Akizungumza na Mwandishi wetu wa Michuzi Blog, Kaimu Mkuu wa Idara ya Ujenzi wa Nguvu ya Pamoja na Harakati, Florah Ndaba Amesema Kuwa mabadiliko ya Sheria, ambazo zilifanyiwa marekebisho na nyingine zimeundwa na zimebeba masuala ya kijinsia na hata TGNP isipokuwepo sheria hizo zitakuwepo.


Florah Amesema kutimiza miaka 30 ya TGNP, wanajivunia kutangaza na kusambaza bajeti yenye mrengo wa kijinsia. "Tunaona serikali imeanza kutenga bajeti zenye mrengo wa kijinsia na tunajivunia kutoa mafunzo kwa wafanyakazi wa serikali kupata mafunzo ya juu bajeti ya mrengo wa kijinsia.
Amesema kuwa TGNP ndio mwanzilishi wa Kampeni ya Mtue Mama Ndoo Kichwani ambayo enaendelea kutekelezwa na Wizara ya Maji inayoongozwa na Jumaa Aweso mbapo mikoa mbalimbali wamenufaika na kampeni hiyo.


Amesema kuwa kampeni hiyo iliungwa mkono na taasisi, Mashirika na kampuni kwa kuchimba visima, kutengeneza matenki ya kuhifadhia maji pamoja na usambazaji mabomba ili kuisaidia jamii kupata maji kwa urahisi.


Hata hivyo kampeni hiyo imekuwa mkombozi kwa Mwanamke ambaye alionekana kuwajibika zaidi katika majukumu ya nyumbani.


Pia amesema kuwa Kampeni hiyo imeweza kumsaidia mwanamke kupunguza muda na umbali wa kutafuta maji hivyo nguvu imeelekezwa kujiinua kiuchumi kwa mwanamke.


Amesema pia mafanikio mengine ni kuwa na vuguvugu la kubadilisha sheria ya Ndoa. Marriage Act katika katiba ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania ni kitu kilichoanza tangu zamani juu ya kutetea mtoto wakike kutokuolewa akiwa chini ya miaka 18.


Sheria hiyo pia imekuwa ikipigiwa kelele na Taasisi pamoja na mashirika mbalimbali ya kutetea haki za mtoto.


Mswada wa mabadiliko ya sheria hiyo yalifika mpaka bungeni na kujadiliwa, hiyo ni moja ya kampeni zilizoanzishwa na TGNP.
“Mabadiliko ya sheria ya likizo ya uzazi nayo ni mafanikiao ambayo wanapata watu wengine ingawa waliopigania mabadiliko ya sheria likizo ya uzazi kwa wanaojifungua ni kitu ambacho hakikuwepo lakini leo hii akinamama wanafaidika juu ya sheria hiyo.”


Pia amesema kuwa kulikuwa na kampeni ya rasilimali ziwanufaishe wanachi, kwa sasa kweli tunaona rasilimali zinawafikia wananchini kwa njia mbalimbali.


Rasilimali zinawafikia wananchi kwa uwepo wa hosptali, zahanati na shule katika mikoa yote hapa nchini.


Ingawa kampeni nyingine hazikuendeshwa na TGNP peke yake lakini wadau mbalimbali walisukuma kampeni hizo mbele mpaka kufikia malengo endelevu ya Milenia.


Licha ya kuwa na Mafanikio hakukosi changamoto Florah amesema kuwa kumekuwa na changamoto ya kuwepo kwa sheria ambazo hazitekelezwi, kwani kazi kubwa imefanyika katika marekebisho ya sheria lakini hazitekelezwi.
Pia amesema Mila na destuli mbaya nazo ni changamoto inaendelea kushikiliwa na baadhi ya makabila na zinarudisha nyuma kazi kubwa inayofanywa na wadau mbalimbali pia zinakwamisha kujikwamua Mwanamke kiuchumi.


Changamoto nyingine ni 'nani anabeba ajenda’, ajenda inabebwa na mtu au na watu, kuna wakati ajenda inabebwa na watu ambao sio wengi ambayo inafanya kutokuwa na mabadiliko ya haraka ya Mtazamo, fikra na kitabia za watu.


Pia Mabadiliko ya uongozi. Amesema kuwa viongozi wanaukuwa katika sekta flani wanatofautiana vipaumbele na kushindwa kubeba ajenda iliyopo na kuanza na ajenda nyingine.


Frola amesema kuwa Changamoto nyingine ni Ukuaji wa Sayansi na Teknolojia, mabadiliko ya teknolojia yameleta shida ukilinganisha na zamani ambapo mtoto alikuwa anajifunza kwa jamii inayomzunguka peke yake, lakini kwa sasa mafunzo yanatoka katika kila pande ya dunia.


"Kwahiyo lazima tueleze kinagaubaga kuwa kunachangamoto za dunia kuwa kijiji na mafanikio ya dunia kugeuka kuwa kijiji, hasa kwenye utetezi wa haki za watoto, ulinzi wa watoto na utetezi wa jinsia unakuta kunakuwa na changamoto katika kutetea...."
Ongezeko la Ukatili; Frola amesema kuwa changamoto hii inasura mbili
i) Uelewa wa jamii ndio unapelekea kuoongezeka kwa matukio ya ukatili, isingekuwa mchango wa wadau mchango wa TAPO(Vuguvugu) kuibua changamoto, hata mikakati ambayo Serikali inafanya kujenga madarasa, Madawati, kutengeneza mikakati mbalimbali ya kupambana na ukatili.


Amesema ukatili usingekuwepo kama kusingekuwepo na TAPO na wadau kuibua na kueleza kinagaubaga ili kuwepo na njia za kukemea na kuzuia zisiendelee kujitokeza.


Kwahiyo ni kitu cha kufurahia kwamba kazi za TAPO zinaibua changamoto katika jamii na zinachukuliwa hatua.


Pia amesema Changamoto hiyo bado ipo kwani matukio ya unyanyasaji wa kijinsia ni mengi pia amesema mashirika yaliyopo nchini inawezekana hayatoshi katika utatuzi wa changamoto hizo zote zinawezesha kuibua fursa au mbinu mbadala ya jinsi ya kutatua changamoto za kijinsia.


"Mabadiliko sio ya siku moja, mabadiliko ya kifikra ni ya kila siku." Amehitimisha Florah.


This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

KUELEKEA TAMASHA LA 15 LA JINSIA, TGNP YAJIVUNIA MAFANIKIO YA KAMPENI, SHERIA

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×