Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII KUTANGAZA UTALII KUPITIA MICHEZO, YAZIDI KUNG'ARA MASHINDANO YA KAMBA - SHIMIWI

Na Mwandishi Wetu, IRINGA.

Timu ya wanaume ya Wizara ya Maliasili na Utalii imeibuka  mshindi kwenye mchezo wa kamba  kwenye mashindano ya Shirikishio la Michezo la Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) yanayoendelea mkoani Iringa.

Akizungumza mara baada ya ushindi huo, Kapteni wa timu hiyo, Faraja Mmasa amesema ushindi uliopatikana umetokana na maandalizi mazuri ambayo yameisaidia timu hiyo kushinda kwa Seti Mbili Kwa sifuri dhidi ya wapinzani wao TARURA. 

"Nianze kwa kuupongeza uongozi wa Wizara ya Maliasili na Utalii Kwa namna ambavyo walituandaa toka maandalizi mpaka kutuwezesha kufika hapa na kushiriki . Timu imejiandaa vizuri na kama unavyoona leo tulikuwa tunacheza mechi dhidi ya TARURA na tumeshinda ushindi wa seti mbili kwa bila." Amesema Mmasa


Ameongeza kuwa timu hiyo ina uwezo wa kusonga mbele kwa  hatua zinazofuata kwani wao kama wachezaji  wamejipanga vizuri kushindana na hatimaye kusinda kwa  hatua zinazofuata.


‘’ Timu ya Wizara ya Maliasili na Utalii tumeona ni timu ambayo ipo Kwa ajili ya ushindani. Tumejipa kuendelea kusonga mbele kuchukua kikombe " Aliongeza Mmasa.

Naye mchezaji wa timu hiyo Paul Shayo amesema, mashindano hayo yanayoendelea mkoani Iringa ni njia moja wapo ya kuutangaza utalii wa ndani na hivyo wanatumia fursa hiyo vilivyo kuhamasisha  utalii wa ndani

Kwa upande wa mchezaji  Chamganda Hamis amesema, kwa ushindi walioupata wanamshukuru Mungu kwani utawasaidia  katika safari yao ya kuelekea kunyakua vikombe.



This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII KUTANGAZA UTALII KUPITIA MICHEZO, YAZIDI KUNG'ARA MASHINDANO YA KAMBA - SHIMIWI

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×