Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

ZAIDI YA WAGONJWA 1000 WAFANYIWA UCHUNGUZI NA KUPATIWA MATIBABU KAMBI YA MADAKTARI BINGWA TANGA

Mratibu wa Kambi hiyo ambaye pia ni Mhazini wa Chama Cha Madaktari Tanzania Dkt Mathew Shao kulia akiteta wakati wa kambi ya Huduma za Madaktari Bingwa wa uchunguzi wa magonjwa mbalimbali Inayoendelea Kwenye Viwanja vya Mkwakwani Jijini Tanga.

Wananchi wakiendelea kupatiwa huduma mbalimbali wakati wa kambi hiyo inayoendelea kwenye viwanja vya CCM Mkwakwani Jijini Tanga






Na Oscar Assenga, TANGA

ZAIDI ya wagonjwa 1000 wamefanyiwa uchunguzi na kupatiwa matibabu katika kambi ya Huduma za Madaktari Bingwa wa uchunguzi wa magonjwa mbalimbali inayoendelea kwenye viwanja vya Mkwakwani Jijini Tanga.

Kambi hiyo iliyoandaliwa na Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Tanga Mhe. Ummy Mwalimu iliyoanza Septemba 25 mwaka huu na inayotarajiwa kumalizika leo tarehe 27 September ilikuwa ikitoa huduma za kibingwa katika magonjwa mbalimbali.

Akizungumza leo Mratibu wa Kambi hiyo ambaye pia ni Mhazini wa Chama cha Madaktari Tanzania Dkt Mathew Shao alisema mwamko wa wananchi umekuwa kuridhisha kutokana na kuongezeka idadi yao kila siku.

Dkt Shao ambaye pia ni Daktari katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa alitaja magonjwa hayo ya kibingwa ni Moyo,Sukari,Mifupa,Pua/koo,
masikio,wanawake na uzazi,kinywa na meno,watoto ,mfumo wa mkojo(Urojolia) na Macho.

Aliyataja magonjwa mengine ni ya Upasuaji,utoaji wa dawa na vipimo vya sukari,moyo-Echo,ECG,Utrasound,Sickle Cell,Uzito na urefu,hali ya lishe,ukimwi/TB,Ushauri na nasaha na elimu juu ya magonjwa yasiyoambukiza (NCD)



This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

ZAIDI YA WAGONJWA 1000 WAFANYIWA UCHUNGUZI NA KUPATIWA MATIBABU KAMBI YA MADAKTARI BINGWA TANGA

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×