Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

TPDC YATOA MAFUNZO KWA WAANDISHI WA HABARI SHINYANGA KUHUSU MRADI WA EACOP... DC SAMIZI ATAKA TAARIFA SAHIHI

   
 Na Sumai Salumu  & Kadama Malunde - Shinyanga
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Johari Samizi amewataka waandishi wa Habari kuandika habari sahihi na kutoa elimu sahihi kwa wananchi kuhusu mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP).

Akizungumza leo Jumanne Septemba 26, 2023 wakati akifungua mafunzo ya siku moja Kwa Waandishi wa Habari mkoa wa Shinyanga yaliyoandaliwa na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) yaliyolenga kuwajengea uelewa kuhusu mradi wa EACOP, Samizi amesema waandishi wa Habari wana jukumu kubwa la kutoa taarifa sahihi kwa wananchi ili kujua faida za mradi huo.

“Nitoe wito kwa waandishi wa Habari muandike taarifa na Habari sahihi kuhusu mradi,waweze kuufahamu mradi huu, tunaimani kabisa mtaenda kutoa taarifa sahihi kuhusu mradi. Nawasihi mtumie kalamu, kamera zenu vizuri kuhabarisha jami",amesema.

"Serikali inaendelea kutekeleza mradi huu mkubwa kwa manufaa ya Watanzania hivyo ni vyema Watanzania wakaufahamu mradi huu”, ameongeza Mhe. Samizi.

Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kutoka TPDC Marie Msellemu amesema wananchi ambao maeneo yao yamepitiwa na mradi asilimia kubwa wamelipwa fidia ikiwemo kujengewa nyumba za kisasa, huku wakandarasi wazawa wakipata kazi katika mradi huo.

Amesema asilimia 80 ya mradi wa Bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima Uganda hadi Chongoleani Tanga inapatikana Nchini Tanzania,huku mikoa 8 ikiguswa na mradi huo ambayo ni Tanga,Shinyanga,Geita,Tabora,Singida,Kagera,Manyara na Dodoma.

Mratibu wa Mradi wa EACOP kitaifa, Asiadi Mrutu  amesema kuwa mradi huu utagharimu kiasi cha zaidi Dola za Kimarekani  Bilioni 5 na utatekelezwa kwa miezi 24 ( miaka 2) kwanzia Januari 2024 bomba hilo la kusafirisha  mafuta ghafi lenye urefu wa mita 18.

"Huu mradi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima Uganda hadi Chongoleani Tanga nchini Tanzania una jumla ya wanahisa 4 Tanzania ikiwa itatoa mchango wa  fedha za mradi kwa 15%  na mdhabuni wa akiwa ni China Petroleum Pipeline Coperation (CCP) ambaye atajenga kwa luti tatu kwanza ni Uganda-Mtukula Km296, Mtukula-Singida Km614 pamoja na Singida -Tanga km533 ambapo kampuni yetu ndani ya mradi EACOP wanasimamia pia kufuatilia namna ya makampuni ya ndani yatakavyonufaika nahuduma yatakazotoa",amesema.

Afisa Uhusiano TPDC Francis Lupokela amesema TPDC inasimamia miradi mikuu minne(4) ikiwemo wa bomba la mafuta ambapo hivi sasa uko kwenye hatua za ujenzi wa makambi kwenye maeneo mbalimbali yakiwa na jumla ya 14.

"TPDC  inatekeleza mradi huu kwa 15% na unapita kwenye mikoa nane mradi huu una jumla ya kilometa 1443 kwa Tanzania na km1147 sawa na  80% kwa Uganda ni Km 296 Sawa 20% na mpaka Agosti 2023 tumetoa ajira za makundi matatu kwa watu zaidi ya 3619 ikiwemo wazawa wa maeneo husika",amesema Lupokela.

Nao waandishi wa habari  waliopata mafunzo hayo wamesema yamewasaidia kujua kuhusu maendeleo ya mradi huo na faida kwa jamii yote inayopitiwa na mradi pamoja na nchi kwa ujumla.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Johari Samizi akifungua Mafunzo Kwa Waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga Kuhusu Mradi wa EACOP
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Johari Samizi akifungua mafunzo kwa waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga kuhusu Mradi wa EACOP
Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga Greyson Kakuru akizungumza wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga kuhusu Mradi wa EACOP
Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kutoka TPDC Marie Msellemu akizungumza wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga kuhusu Mradi wa EACOP
Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kutoka TPDC Marie Msellemu akizungumza wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga kuhusu Mradi wa EACOP
Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kutoka TPDC Marie Msellemu akizungumza wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga kuhusu Mradi wa EACOP
Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kutoka TPDC Marie Msellemu akizungumza wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga kuhusu Mradi wa EACOP
Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kutoka TPDC Marie Msellemu akizungumza wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga kuhusu Mradi wa EACOP
Mafunzo yakiendelea
Mratibu wa Mradi wa EACOP kitaifa, Asiadi Mrutu akizungumza wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga kuhusu Mradi wa EACOP
Afisa Uhusiano TPDC, Francis Lupokela akizungumza wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga kuhusu Mradi wa EACOP
Afisa Uhusiano TPDC, Francis Lupokela  akizungumza wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga kuhusu Mradi wa EACOP
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano EACOP, Catherine Mbatia  akizungumza wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga kuhusu Mradi wa EACOP
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano EACOP, Catherine Mbatia  akizungumza wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga kuhusu Mradi wa EACOP
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano EACOP, Catherine Mbatia  akizungumza wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga kuhusu Mradi wa EACOP
Afisa Habari EACOP, Abbas Abraham akizungumza wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga kuhusu Mradi wa EACOP
Afisa Habari EACOP, Abbas Abraham akizungumza wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga kuhusu Mradi wa EACOP
Afisa Habari EACOP, Abbas Abraham akizungumza wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga kuhusu Mradi wa EACOP
Afisa Habari EACOP, Abbas Abraham akizungumza wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga kuhusu Mradi wa EACOP
Afisa Fursa kwa Wazawa EACOP, Maryam Mandia akizungumza wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga kuhusu Mradi wa EACOP
Afisa Fursa kwa Wazawa EACOP, Maryam Mandia akizungumza wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga kuhusu Mradi wa EACOP
Mratibu wa Mahusiano ya jamii EACOP Shinyanga, Cecilia Nzeganije akizungumza wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga kuhusu Mradi wa EACOP
Mratibu wa Mahusiano ya jamii EACOP Shinyanga, Cecilia Nzeganije akizungumza wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga kuhusu Mradi wa EACOP




This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

TPDC YATOA MAFUNZO KWA WAANDISHI WA HABARI SHINYANGA KUHUSU MRADI WA EACOP... DC SAMIZI ATAKA TAARIFA SAHIHI

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×