Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

NAIBU WAZIRI BYABATO AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA BIASHARA WA JAMAICA

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Wakili Stephen Byabato(Mb) amekutana na kuzungumza na Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara wa Jamaica Mhe. Kamina John Smith pembezoni mwa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kundi la G77+ China unaofanyika jijini Havana nchini Cuba.

Katika mazungumzo yao viongozi hao wameelezea kuridhishwa kwao na hali ya uhusiano wa kidiplomasia uliopo kati ya Tanzania na Jamaica na kuahidi kuendelea kushirikiana zaidi ili kuimarisha uhusiano huo.

Akizungumza katika kikao hicho Mhe. Byabato amemuelezea Mhe. Smith kuwa Tanzania inaridhishwa na Uhusiano Mzuri Uliopo na kuongeza kuwa kuna haja ya kuhakikisha uhusiano huo wa kidplomasia unaimarishwa na kufikia hatua ya juu.

Amemhakikishia utayari wa Serikali ya Tanzania kuanzisha Tume ya Kudumu ya Pamoja (JPC) na Jamaica katika maeneo yatakayozinufaisha pande zote mbili.

Pia amemuelezea nia ya Tanzania ya kupanua wigo wa maeneo ya ushirikiano na kuingiza sekta za uchumi wa bluu, biashara na uwekezaji.

Naye Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara wa Jamaica Mhe. Kamina John Smith alisema pamoja na uhusiano mzuri uliopo kati yake na Tanzania, Jamaika inaiomba Tanzania kuiunga mkono katika nafasi mbili inazogombea kimataifa katika Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia masuala ya Bahari (IMO) na Kamati ya Urithi wa Dunia iliyoko chini ya UNESCO.


This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

NAIBU WAZIRI BYABATO AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA BIASHARA WA JAMAICA

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×