Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

TAMKO LA KULAANI KUSHAMBULIWA KWA WAANDISHI WA HABARI



 Chama  Cha  Waandishi wa Habari wa Kupiga  Vita  Matumizi  ya  Dawa za  Kulevya na Uhalifu Tanzania  (OJADACT) kinalaani  tukio  la  kijinai  lililofanywa  na  vijana  wa  jamii ya  kimasai  dhidi  ya  waandishi wa  habari lililotekea  Agosti, 15,  2023  katika Kijiji cha  Enduleni, Wilaya  ya  Ngorongoro, Jijini Arusha.
 

Tukio  hilo   lilihusishwa  kujeruhiwa  kwa  Waandishi wa  habari    wafuatao, Ferdnand   Shayo  (ITV), Dennis  Msacky (Media  Brain),Habib  Mchange (Jamvi  la  Habari),Elia  Kinian (Channel  Ten),Janeth  Joseph (Mwananchi), Dickson Busagaga (Clouds   Media)  na  Mkalimani  wao  Lengai  Ngoishiye,

 

Waandishi  hao  walikutwa  na madhila  hayo   wakati  wakitekeleza  majukumu  yao  ya  kikazi ya  kutafuta  taarifa za  wamasai wanaoishi  Ngorongoro   na  kutaka  kuhama   kwa  hiari  yao  toka  Kijiji cha  Enduleni kilichopo  ndani  ya  hifadhi  ya  Ngorongoro.

 

OJADACT  inaamini   kuwa  Jeshi la  Polisi  Mkoa wa Arusha  pamoja na Mamlaka  nyingine  za  ulinzi  na usalama    zitawatafuta  na  kuwakamata  watuhumiwa  wa  tukio hilo  na kuwafikisha  kwenye   mkono wa  sheria  ili  wawajibishwe na  iwe  funzo  kwa  watu  wengine  wenye  nia  ovu  dhidi  ya  waandishi wa  habari.

 

Pia  OJADACT inawakumbusha  waandishi wa  habari  na  vyombo  vya  habari  kufanya  tathimini  ya  ulinzi  na  usalama  wa  maeneo  wanayotakiwa  kwenda  kufanya  kazi  zao  ili  kupungunza  madhila  yanayoweza  kuwapata  na  pia  OJADACT inatia  pole  majeruhi  wote.

 

 Edwin  Soko

 Mwenyekiti,  OJADACT

 Julai Agosti 17, 2023



This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

TAMKO LA KULAANI KUSHAMBULIWA KWA WAANDISHI WA HABARI

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×