Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

WAKULIMA WAIMWAGIA SIFA BENKI YA CRDB MBELE YA RAIS SAMIA


Rais Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akipata maelezo mafupi kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Kilimo Biashara wa Benki ya Crdb, Ndugu Maregesi Shaaban alipotembelea Banda la Benki ya CRDB katika kilele cha maadhimisho ya Nanenane yaliyofanyika kitaifa Jijini Mbeya. Wakishuhudia ni Spika wa Mbunge Mh. Dkt. Tulia Ackson na Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya CRDB, Ndungu Fredrick Nshekanabo.
BAADHI ya wakukima mkoani Mbeya wameishukuru Benki ya CRDB mbele ya Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuwa imewasaidia kupata mikopo ya fedha na nyenzo ikiwemo trekta aina ya Power Tiller, kuwa vitawasaidia kuinua kilimo na kupata kipato.


Mmoja wa wakulima hao kutoka Wilaya ya Mbalali mkoani Mbeya Halima Ally, ametoa ushuhuda huo leo mbele ya Rais Dkt. Samia alipotembelea Banda la Benki ya CRDB kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo (Nane Nane) yaliyofanyika kwenye Viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya.


"Sisi wakulima wa Mbarali tunaishukuru Benki ya CRDB kwa kutuwezesha kupata mikopo ya fedha na zana za kufanyia kazi kama ilivyotukopesha Power Tiller. Kwa kupata Power Tiller hii itaniwezesha kuendeleza kilimo changu cha mpunga na mahindi" alisema Ally.
Wakulima zaidi ya 600 kutoka Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya wanatarajiwa kukopeshwa na Benki ya CRDB trekta, power tiller, zana za kuvunia, fEdha za mikopo ya kulimia na pembejeo za kilimo ikiwemo mbegu, mbolea na madawa, na mikopo ya Stakabadhi Ghalani.


Rais Dkt. Samia, aliipongeza Benki ya CRDB kwa kuweza kukopesha wakulima kwa riba ya asilimia tisa, huku akiitaka benki hiyo kuendelea kufuatilia l zana za kilimo wanazowakopeaha wakulima ili ziendelee kufanya kazi, na ikibidi kuwasaidia kutengeneza pindi zinapoharibika, kwani baadhi yao zana hizo zikiharibika, wanazitelekeza.


"Nawapongeza CRDB kwa kuweza kutoa mikopo ya riba ya asilimia tisa. Itawasaidia wakulima kuweza kukopa kwa wingi na kulima kwa tija.


"Na mikopo ya Power Tiller mnayotoa kwa wakulima muweze kuifuatlia na muwasaidie au kuweza kuwasaidiia waweze kutengeneza. Wakati mwingine power tiller linaharibika na kulitelekeza hivyo kushindwa kuleta tija" alisema Rais Dkt. Samia.


Awali, Mkuu wa Kitengo cha Kilimo Biashara wa Benki ya CRDB Maregesi Shaaban alisema Benki ya CRDB imeendelea kutoa mikopo inayofikia sh. trilioni 3.9 kwa misimu mitano iliyopita hadi kufikia Julai, 2023, sawa na asilimia 43 ya mikopo yote itolewayo na mabenki kwenye Sekta ya Kilimo na Mifugo hapa nchini.


"Tunatoa mafunzo kwenye vituo atamizi chini ya mpango maalum wa BBT kupitia Wizara ya Kilimo na Wizara ya Mifugo na Uvuvi. Tunaendelea kutoa elimu ya fedha na usimamizi wa miradi kwenye vituo vilivyoko kote nchini. Uwezeshaji vijana na wanawake kwenye kilimo, uvuvi, mifugo, viwanda na biashara Bara na Visiwani.


"Benki ya CRDB kupitia kampuni yetu tanzu ya CRDB Bank Foundation, inawekeza kwa vijana na wanawake ili waweze kutimiza ndoto zao ikiwa ni pamoja na kuwapa mafunzo na kuwapatia mitaji kwa ajili ya uanzishaji wa miradi mipya (startup capital).


Mitaji hii hutolewa kwa vijana na wanawake wenye mawazo bunifu kibiashara, na Benki ya CRDB inatoa mitaji ya awali ikiwa ni mbegu itakayoleta matunda na kuwafungulia kesho yao yenye tija zaidi kiuchumi, chini ya program ya kipekee ijulikanayo kama IMBEJU".alisema Shaaban.


Shaaban alisema Benki ya CRDB imefanikiwa kufufua matumaini ya wana ushirika kwa kuongezea mtaji inayofikia sh. bilioni 10.2, ambapo sh. bilioni 3.2 kwa TACOBA na sh. bilioni 7.0 kwa KCBL. Taasisi hizo zilikuwa zikijiendesha kwa hasara na baada ya kupata mtaji na usimamizi madhubuti kutoka Benki ya CRDB, zimeanza kujiendesha kwa faida kubwa na kutokana na mikakati madhubuti ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia, wanaendelea kutekeleza ndoto nzuri ya kiuchumi ya uanzishwaji wa Benki ya Ushirika ya Taifa.


Shaaban alisema, Benki ya CRDB ikishirikiana na wauzaji wa vifaa madhubuti vya kilimo (Agricom), imeweza kuwakabidhi baadhi ya wanufaika waliopata mikopo ya kununua Power Tillers kwa ajili ya kilimo cha mpunga mkoani Mbeya.


"Benki ya CRDB itaendelea kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kuendeleza fursa za uwekezaji zilizopo Bara na Visiwani.


Tunawakaribisha wadau wote walipo ndani na nje ya nchi yetu ya Tanzania wafike kwenye matawi yetu yaliyoko kote nchini na kwenye nchi jirani za Burundi na Congo DRC ili tuweze kuwahudumia.


"Tunatoa Shukran za dhati kwa Business Units zote za CRDB na uongozi wa Benki yetu pendwa ya CRDB (kipekee tunatoa Shukran kwa our MD&Group CEO, CCO, COO, CFO, DCA, DCB, DRB, DC, DCA, MD-CRDB BANK FOUNDATION & the entire CRDB MARKETING TEAM) kwa kutuwezesha vilivyo hadi kufikia kilele cha maadhimisho haya ya Maonesho ya Nane Nane kitaifa mkoani Mbeya kwa mafanikio makubwa" alisema Shaaban.

--


This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

WAKULIMA WAIMWAGIA SIFA BENKI YA CRDB MBELE YA RAIS SAMIA

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×