Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

TAASISI YA BILAL MUSLIM YATUMIA KUMBUKIZI YA KIFO CHA MJUKUU WA MTUME (S.A.W) KUCHANGIA DAMU HOSPITALI YA RUFAA BOMBO

 










Na Oscar Assenga, TANGA.

WANAFUNZI, walimu pamoja na waumini wa dini ya Kiislamu zaidi ya 130 kutoka Taasisi ya Bilal Muslim Mission of Tanzania Tawi la Tanga wametumia maadhimisho ya mwaka mpya wa kiislamu ulioambatana na kukumbukizi ya kifo cha Mjuu wa Mtume (S.A.W) Imam Hussein Ally Kuchangia Damu salama katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo

Mkuu wa shule ya Wasichana katika taasisi hiyo Sheikh Sajad Hassan akizungumza mara baada ya zoezi hilo alisema kuwa uchangiaji wa Damu katika hospitali hiyo kawaida yao ya kila mwaka ikiwa ni ishara ya kuonesha moyo wa kujitolea wahitaji mbalimbali hususani watoto na mama wajawazito waliopo hospital wanaohitaji kuongezewa damu.

Mbali na kuchangia damu lakini pia waliwatembelea kwenye wodi ya wakina mama wajawazito na kugawa zawadi mbalimbali kwa wagonjwa ikiwa ni sehemu ya kuwafariji.

Alisema kusudio la wao kuchangia damuni kujitolea sadaka ambayo wanaifungamanisha na na tukio la kuwawa kwa mjukuu wa bwana mtume (S.A .W) Hussein Bin Ally aliyeuwawa mwaka 61 Hijiria huko Irak aliyekuwa wakiipigania dini kwa lengo la kukemea mabaya na kuamrisha mema, aliyetoka kutetea wanyonge na wale waliodhulumiwa

Aidha alisema wao kama taasisi wamejiwekea utaratibu wa kufanya zoezi hilo kila mwaka katika maeneo tofauti tofauti lengo ni kuonyesha kwamba wamesimama pamoja na mjukuu wa bwana mtume (S.A.W) katika kutetea wanyonge.

“Tunaimani kwamba damu hii itasaidia wanyonge, pia tunasimama na kukemea dhuluma zozote zinazoendelea ulimwenguni" alisema Sheikh Hassan.

Awali akizungumza wakati wa zoezi hilo Mkuu wa Idara ya Maabara katika Hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Sinde Ntobu ameishukuru Bilal Muslim kwa kuona kuwa wanayo nafasi kubwa kuokoa maisha ya watu wanaofika hospitalini hapo kupatiwa huduma ikiwemo kuongezewa damu.

Alisema uhitaji wa damu kwa mwezi katika hospital hiyo ni mkubwa tofauti na ile inayochangiwa ambapo uhitaji wao unafikia lita 500 hadi 600 wakiwa na upungufu wa damu kwa Unit 250 hadi 300 hivyo kuziomba taasisi na watu binafsi kuona umuhimu wa Kuchangia Damu Ili kuokoa maisha ya watu.

" Sisi kama hospital kwa wastani kwa mwezi tunatumia chupa za damu 500 mpaka 600 lakini uwezo wa kuchangia damu ambayo inapatikana mara nyingi tunapata unit 250 mpaka 300 kwahiyo uhitaji wa damu kwa wagonjwa ni mkubwa "Alisema Mtobu

Hata hivyo aliiasa jamii kuona umuhimu wa kuchangia damu ili kuweza kuokoa maisha ya wengine wahitaji lakini baadae zinaweza kuwasaidia wanapokuwa wahitaji.


This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

TAASISI YA BILAL MUSLIM YATUMIA KUMBUKIZI YA KIFO CHA MJUKUU WA MTUME (S.A.W) KUCHANGIA DAMU HOSPITALI YA RUFAA BOMBO

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×