Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

WATOTO WALIOWEKA REKODI GGML KILICHALLENGE, WANG'ARA SIKU YA MASHUJAA

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge, Jenista Mhagama (katikati) akiwa Abeli Mussa (kushoto) na Rebecca Damian (kulia) baada ya kuwapokea wanafunzi hao walioshiriki kupanda Mlima Kilimanjaro kupiti kampeni ya GGML KiliChallenge -2023 inayolenga kuhamasisha uchangishaji wa fedha za mapambano dhidi ya VVU/Ukimwi.


Na Mwandishi wetu

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), Jenista Mhagama amewapongesa Watoto Abel Mussa na Rebbeca Damian wenye umri wa miaka 14 waliopanda mlima Kilimanjaro kupitia kampeni ya GGML KiliChallenge- 2023, huku watoto hao wakibainisha kuwa hatua yao hiyo ililennga kuunga mkono jitohada za Rais Samia Suluhu Hassan hususani katika kuwajali watoto nchini.

Watoto hao wanaolelewa na Kituo cha Moyo wa Huruma kilichoazishwa na kufadhiliwa na Kampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML), walikuwa ni moja ya washiriki 61 waliopanda mlima Kilimanjaro tarehe 14 Julai 2023 na kushuka tarehe 20 Julai mwaka huu.

Washiriki hao walipanda mlima huo kupitia kampeni ya GGML KiliChallenge anayolenga kukusanya fedha za kuendeleza mapambano dhidi ya VVU/ Ukimwi.

Akizungumza katika maadhimisho ya siku ya kumbukumbu ya mashujaa juzi tarehe 25 Julai 2023 jijini Dodoma, Mhagama alisema watoto hao walimuambia wamepanda mlima huo kwa kuzingatia kazi kubwa anayofanya Rais Samia Suluhu Hassan ya ulinzi wa watoto wa kitanzani, haki zao na ustawi wao.


"Vilevile kwa kazi kubwa iliyofanywa na Serikali katika ujenzi wa miundombinu ya elimu ya msingi na sekondari na vyuo vikuu. Lakini pia wamesema walipanda kwa kuzingatia kazi kubwa unayofanya kwenye miundombinu ya afya haya yote yakiwa na ustawi mkubwa wa watoto wote wa Tanzania," alisema.


Amesema mbali na kushirikiana na serikali kusaidia mapambano dhidi ya tatizo la Ukimwi, pia watoto hao ambao ni wanafunzi wa darasa la saba, walipanda mlima huo kwa lengo la kuanzisha moyo wa uzalendo kwa watoto wengine ili watambue kuwa nchi sasa inaoongozwa na rais ambaye anajali ustawi wa watoto.


Kati ya watoto hao, Rebecca Damiani ambaye ni mwanafunzi katika Shule ya Msingi Kivukoni- Geita, alifika katika kilele cha Uhuru cha mlima huo, huku Abel Mussa ambaye ni mwanafunzi wa shule ya msingi Mbugani pia kutoka mkoani Geita, alirudia njiani baada ya kuugua malaria.


Kampeni hiyo iliyoasisiwa na GGML mwaka 2002 kwa kushirikiana na Tume ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS), mwaka huu ilishirikisha wapanda mlima 35 na waendesha baiskeli 26 waliouzunguka mlima Kilimanjaro kwa siku saba.


Akiwapokea washiriki hao, tarehe 20 Julai mwaka huu, Mhagama alimwagiza Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo kuhakikisha wanafunzi hao wanaingizwa kwenye orodha ya miongoni mwa watu watakaohudhuria sikukuu ya mashujaa ambayo imefanyika juzi tarehe 25 Julai 2023.


This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

WATOTO WALIOWEKA REKODI GGML KILICHALLENGE, WANG'ARA SIKU YA MASHUJAA

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×