Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

MAFUNZO MAALUMU YA MATIBABU YA UTAPIAMLO MKALI KWA WATOTO YATOLEWA KWA WATUMISHI HOSPITALI YA RUFAA YA BOMBO

 Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Mohamed Salehe wa tano  kulia mwenye koti akifuatilia kwa umakini  Mafunzo Maalumu yanayohusu matibabu ya utapiamlo mkali kwa watoto yametolewa kwa watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo

Sehemu ya washiriki wa mafunzo wakifuatilia 
Daktari wa Wodi ya Watoto katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga -Bombo Dkt Mwalimu Khalid



Na Oscar Assenga,TANGA.

MAFUNZO Maalumu yanayohusu matibabu ya utapiamlo mkali kwa watoto yametolewa kwa watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo huku yakielezwa kuwa yatakuwa na umuhimu mkubwa kwao.

Akizungumza wakati akifungua mafunzo hayo ya siku mbili,Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Mohamed Salehe alisema mafunzo hayo yatawasaidia kuongeza ufanisi wakati wa utoaji wa huduma kwa wagonjwa.

Dkt Mohamed ambaye pia ni Mkuu wa Idara ya Watoto katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga alisema baada ya kumalizika kwa mafunzo hayo anaimani kwamba washiriki wanakwenda kuwa chachu katika utoaji wa huduma.

Mafunzo hayo yamewashirikisha wataalamu mbalimbali wakiwem kutoka Ustawi wa Jamii, Madaktari, Manesi na maafisa lishe ambayo yanatajwa kwamba yatakuwa chachu katika utoaji wa huduma

Alisema mafunzo hayo yanatolewa kwa natharia na vitendo huku washiriki wakionekana kuwa na uelewa mzuri na walimu wamekuwa wakitoa mafunzo ya kuwaezesha kutoa matibabu kwa watoto wenye utampiamlo.

“Unampomtibu mtoto mwenye tatizo la utapiamlo linahitaji watu wote waweze kusaidiana na chimbuko la hasa na sababu kuweza kujulikana na kumtibu ndio moja njia pekee ya kuweza kumuondolea huyo mtoto tatizo hilo”Alisema

Dkt Mohamed alisema akiwa ametibiwa Hospitali lakini pia akirudi nyumbani awe ametibika moja kwa moja ikiwemo kupewa matunzo wanaporudi nyumbani baada ya kumaliza matibabu.

“Pamoja na kwamba wanatibiwa Hospital wanahitaji matunzo huko nyumbani watoto wanakaa na wazazi hivyo ni kuwapa mafunzo ya namna ya kuwalea watoto kama hao kwani wanaweza kuwa kama wengine na ndoto zao ila mafunzo kwa wazazi ni jambo la muhimu”Alisema

Awali akizungumza wakati wa mafunzo hayo Afisa Lishe wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga –Bombo Imakula Mwamrefu alisema wapo kwenye mafunzo maalumu yanayohusu matibabu kwa watoto wenye utapiamlo mkali wanaozaliwa katika hospitali hiyo.

Alisema kwamba kwenye hospitali hiyo wana kitengo ndani ya wodi ya watoto 13 na 14 kinachohusika kwa matibabu ya utapiamlo mkali kwa watoto hivyo kutokana na hilo wameona wawe na mafunzo ya kujengeana uwezo namna ya kuwatibu watoto wanapofika hospitalini.

Hata hivyo alisema kwamba mafunzo hayo yatakuwa kwa njia ya kuelekezana na vitendo kuona namna ya kutambua utapiamlo mkali

Naye kwa upande wake Daktari wa Wodi ya Watoto katika Hospitali hiyo Dkt Mwalimu Khalid alisema kwamba mafunzo hayo ya matibabu kwa watoto wenye utapiamlo mkali ni muhimu kutokana na kwamba wanakuwa na miili yenye mabadiliko hivyokuna na utofauti jinsi ya kuwatibu ukilinganisha na wale wa kawaida.

Alisema hiyo kuna umuhimu wa madaktari na manesi wanaopokuwa na wajibu wa kuwaangalia hao watoto wanatakiwa kueleza mafunzo hayo kutokana na watoto hao wanatibiwa tofauti na wengine hivyo daktari anaweza kuwa mzuri sana kutibu watoto lakini akimpata mtoto kama huyo kama hajapata mafunzo anaweza kumtibu tofauti.


This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

MAFUNZO MAALUMU YA MATIBABU YA UTAPIAMLO MKALI KWA WATOTO YATOLEWA KWA WATUMISHI HOSPITALI YA RUFAA YA BOMBO

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×