Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

NDERIANANGA AWATAKA WATANZANIA KUUNGA MKONO JUHUDI ZA RAIS SAMIA

 




Na Mathias Canal, Moshi-Kilimanjaro

Mbunge wa Viti maalumu Mhe Ummy Nderiananga ambaye pia ni Naibu waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge) akiwa katika ziara mkoani Kilimanjaro amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan Kwa imani kubwa aliyompatia ya kumteua kuwa Naibu Waziri.

Akizungumza Katika mkutano na wananchi uliofanyika katika kijijini kwao Lotima ambapo ndipo alipozaliwa katika Kata ya Makuyuni ambapo ameeleza umuhimu wa shule za kata katika kuimarisha elimu nchini kwani zimeongeza chachu ya mafanikio kwa wananchi ambapo ametolea mfano yeye ambaye alisoma katika shule hizo.

Amesema kuwa Rais anafanya kazi usiku na mchana hivyo watanzania wanapaswa kumtia moyo na kumuunga mkono ili aweze kufikia dhamira ya kuwaletea maendeleo endelevu.

"Mhe Rais Samia ana upendo mkubwa na wana Kilimanjaro na sisi wanamakuyuni tumeona upendo wake, tumeona kujali kwake na kuthamini kwake" Amekaririwa Mhe Nderiananga.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Vunjo Mhe Dkt Charles Kimei amemshukuru Rais Samia kwa kuendelea kuboresha huduma mbalimbali za maendeleo ikiwemo utengenezaji wa barabara ya Himo-Makuyuni kwa kiwango cha lami ambayo imeshaanza kutengenezwa.

Amesema kuwa ujenzi wa barabara hiyo utarahisisha huduma za kijamii ikiwemo usafirishaji wa mazao ya chakula na biashara.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Moshi Mhe Kisare Makori ameshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan Kwa miradi mingi ya maendeleo katika Wilaya ya Moshi.





This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

NDERIANANGA AWATAKA WATANZANIA KUUNGA MKONO JUHUDI ZA RAIS SAMIA

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×