Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

CHONGOLO ATUA MBEYA KUFANYA MKUTANO WA HADHARA, KUULEZEA UENDELEZAJI BANDARI DAR


Na Mwandishi Wetu, Mbeya

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Daniel Chongolo amewasili katika Uwanja wa Ndege wa Songwe jijini Mbeya, tayari kwa kufanya mkutano mkubwa wa hadhara utakaofanyikaUwanja wa Luanda jijini humo.

Chongolo akiwa uwanja wa ndege amelakiwa na viongozi mbalimbali wa chama na Serikali wa mikoa jirani pamoja na Spika wa Bunge Dk. Tulia Ackson ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini.

Katika mkutano huo pamoja na mambo mengine Chongolo ataelezea hatua kwa hatua usahihi wa makubaliano ya uendeshaji wa Bandari ya Dar es Salaam, lengo likiwa kuhakikisha bandari hiyo inatoa huduma kwa viwango vya hali ya juu tofauti na ilivyo sasa.

Kwa mujibu wa ratiba ,mkutano huo utahudhuriwa pia na baadhi ya wananchi kutoka mikoa ya Iringa, Njombe, Songwe na Rukwa.



This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

CHONGOLO ATUA MBEYA KUFANYA MKUTANO WA HADHARA, KUULEZEA UENDELEZAJI BANDARI DAR

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×