Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

TANZANIA MWENYEJI MKUTANO WA AGRF 2023

 

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdalla Ulega Akizungumza na Waandishi wa habari Jijini Dodoma kuhusu Mkutano wa AGRF 2023.
Na Dotto Kwilasa, Dodoma

Zaidi ya washiriki 3000 wanaojihusisha na mnyororo wa thamani wa Mifugo na chakula wanatarajiwa kuhudhuria mkutano wa kimataifa wa sekta ya Mifugo na uvuvi (AGRF-2023) ifikapo September 5-8,2023 Jijini Dar Es Salaam.

Akizungumza na Waandishi wa habari leo Julai 14,2023Jijini hapa,Waziri wa Mifugo na uvuvi Abdalla Ulega amesema Tanzania inaenda Kuwa mwenyeji wa mkutano huo hivyo Ushiriki wa wadau wa kisekta watanufaika na fursa zitakazopatikana ikiwemo kukutana na wafanyabiasha mashuhuri na wawekezaji kutoka nchi mbalimbali hali inayotazamwa kufungua milango ya uwekezaji na mashirikiano kibiashara.

"Lengo ni kuwezesha vijana na wanawake kushiriki kikamilifu kuingia kwenye ufugaji na uvuvi na kuwa na uwezo wa kusafirisha Mifugo hai nje ya nchi na kuitangaza nchi,ili kurahisisha hayo Serikali inaendelea kuboresha utaratibu wa upatikanaji wa vibali vya kusafirisha Mifugo na mazao yake nje ili kuleta unafuu kwa wafugaji,"amesisitiza

Waziri Ulega amesema mkutano huo utatoa fursa ya kuongeza uzalilishaji na kukidhi mahitaji ya soko la ndani na kuuza ziada ya mazao na kufafanua kuwa kwa sasa biashara ya nyama imeshamiri na kuuza tani 12,000 kwa mwaka sawa na Dola za marekani milioni 51 ambapo kabla ya hapo Tanzania iliuza tani 1600 pekee .

"Lazima tufuge Kwa malengo,wafugaji wanapaswa kuelewa kuna kuishi na kuku na kufanya biashara ya kuku, tuingie kwenye kufuga mifugo biashara na sio kuiishi na Mifugo kama wengi wanavyofanya huko vijijini,"amesema na kuongeza;

"Sisi kama Serikali tulianzisha mkakati wa mashamba darasa Kwa halmashauri 44 zenye Mifugo Kwa kuanzisha mashamba zaidi ya 100 Ili kuwaonesha wafugaji kuwa inawezekana kulima,kuvuna na kuhifadhi Kwa faida zaidi,hii itaenda sambamba na urasilimishaji wa Kilimo cha majani na uhifadhi wa ardhi,pomoja na kuwa na Ranchi za asili,"amesisitiza

Waziri huyo pia ametumia nafasi hiyo kuwakumbusha wadau kuandaa taarifa za Kampuni zao kwa ufasaha ili iwe rahisi kujitangaza na kuvutia wawekezaji,wafadhili na kuongeza wigo wa biashara zao.


This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

TANZANIA MWENYEJI MKUTANO WA AGRF 2023

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×