Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

WAZIRI PROFESA MKENDA ASIFU UBUNIFU UNAOFANYWA NA TAASISI YA TOIO



Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda akiendesha moja ya baiskeli ya magurudumu matatu iliyotengenezwa na kubuniwa na Taasisi ya Tanzania Open Innovation Organization (TOIO) wakati wa ziara yake


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda akiendesha moja ya baiskeli ya magurudumu matatu iliyotengenezwa na  kubuniwa  na Taasisi ya Tanzania Open Innovation Organization (TOIO) wakati wa ziara yake  kushoto ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Tanzania Open Innovation Organization (TOIO) Shaukatali Hussein 

 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda kushoto akiteta jambo na Mkurugenzi wa Taasisi ya Tanzania Open Innovation Organization (TOIO) Shaukatali Hussein  kulia wakati wa ziara yake

Na Oscar Assenga,Tanga

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda amesifu ubunifu unaofanywa na Taasisi ya Tanzania Open Innovation Organization (TOIO) ya kubuni vifaa mbalimbali vya umeme ikiwemo Baiskeli na Pikipiki huku akihaidi kuunga mkono juhudi hizo.

Profesa Mkenda aliyasema hayo wakati alipoitembelea Taasisi hiyo wakati wa ziara yake ya kutembelea Mradi wa pikipiki za umeme,baiskeli ambazo zinazoziunda wenye shule ya Sekondari Tanga Ufundi.

Akiwa katika eneo hilo Waziri Profesa Mkenda alizitaka taasisi zinazojihusisha na teknolojia na ubunifu kuwasaidia wabunifu nchini kuweza kuzalisha bidhaa zenye ubora.

Alisema kwamba kupitia ubunifu ambao unafanywa na taasisi kama TOIO wanaweza kuona namna ya kupata bajeti ambayo wanaitumia kuweza kuitumia kwa ajili ya kununua hivi vitu ili kuwaunga mkono watanzania ambao wanabuni vitu mbalimbali vyenye manufaa.

“Kupitia bajeti hiyo tutaitumia kununua hivi vitu vinavyotengenezwa hapa kitu kimoja tutangeneza mfumo wa kuvifabrikate kwa scale ya haraka”Alisema

Waziri Mkenda alisema kwamba vipaumbele vyao kwa bajeti iliyopo ya serikali ni kuona namna ya kuwasaidia wabunifu hao kununua hivi vitu tayari na serikali itanunua.

Awali akizungumza Mwakilishi wa Botna Foundation  Dkt Hassan Mshinda alisema wao walipata ufadhii wa kujenga ujuzi huo sio kwa wanafunzi tu bali na jamii ya nje.

Alisema  wanachofikiria ile integration kwenye mafunzo kama hayo ni fursa nyengine nzuri wanaweza kuona namna ya kupatna pamoja

Naye kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Tanzania Open Innovation Organization (TOIO) Shaukatali Hussein alisema  wamekuwa wakitoa ujuzi jinsi ya kutengeneza na kurekebisha vifaa mbalimbali ikiwemo pikipiki za umeme na baiskeli nia ikiwa na ya kuwa mjasiriamali anaweza kutengeneza pia



This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

WAZIRI PROFESA MKENDA ASIFU UBUNIFU UNAOFANYWA NA TAASISI YA TOIO

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×