Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

WATUMISHI WA KANDA YA KUSINI MTWARA WATAKIWA KUWA WAADILIFU




Kamisha wa Maadili Mh Jaji Sivangilwa Mwangesi aliyekaa katikati kushoto kwake ni Katibu Msaidizi Kanda ya Kati kusini Bw Philoteus Manula na kulia kwake ni Afisa Tawala Bw Steven Jarka wakiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Sekretarieti Kanda ya Kusini Mtwara Ikiwa ni maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma mkoani Mtwara tarehe 21 Juni 2023.


Kamishna wa Maadili Mh Jaji Sivangilwa Mwangesi katika akiwa katika ziara yake kutembelea ofisi ya Kanda ya Kusini Mtwara ikiwa ni maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma tar 21 Juni 2023

Na.Mwandishi Wetu Watumishi wa Kanda ya Kusini Mtwara, wametakiwa kutekeleza majukumu yao kwa Uadilifu, umakini na weledi wa kiwango cha juu.

Kauli hiyo imetolewa na Kamishna wa Maadili Mh Jaji Sivangilwa Mwangesi katika ziara yake ya kutembelea Kanda hiyo tar 21 June 2023.

Aisha, Jaji Mwangesi katika hotuba yake ameongeza kuwa ziara hiyo ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma iliyoanza rasmi tar 16 June na kuhitimishwa tar 23 June 2023.

Mhe, Kamishna alifafanua kuwa , lengo kubwa la ziara yake katika maadhimisho haya ni kuwakumbusha watumishi wa Umma na viongozi kwa ujumla kuhusu wajibu wao, na maadili katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku.

Kuhusu changamoto zilizopo katika kanda hiyo, Mh Mwangesi alifafanua kuwa kuhusu uhaba wa watumishi na upungufu wa magari suala hilo linafanyiwa kazi na mchakato unaendelea.

Mh Mwangesi amewataka watumishi wa Kanda ya Kusini Mtwara kutunza jengo la Maadili ambalo ni zuri na kubwa ili liweze kudumu kwa muda mrefu ikiwa ni sehemu ya uboreshaji wa mazingira ya kafanyia kazi.

Aliongeza kuwa Sekretarieti iko katika mchakato wa kuanzisha mfumo wa Online Decrelation Syterm (ODS) ambao utasaidia kurahisisha utekelezaji wa majukumu ya Taasisi na pia kuwawezesha viongozi kutuma matamko yao kwa njia ya Mtandao kwa uhakika na urahisi zaidi tofauti na ilivyo sasa.

Ziara hii ya Mh Kamisha wa Maadili katika kanda ya kusini Mtwara ikiwa ni maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma kitaifa iliyoanza rasmi tarehe 16 juni na kuhitimishwa tar 23 junior, 2023.


This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

WATUMISHI WA KANDA YA KUSINI MTWARA WATAKIWA KUWA WAADILIFU

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×