Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

BIBI HARUSI AZUA GUMZO KUVAA SHELA YA RANGI NYEUSI KWENYE HARUSI YAKE

Bibi harusi kutoka Nigeria kwa sasa anavuma kwenye mitandao ya kijamii baada ya picha zake za harusi kusambaa mtandaoni.

Katika picha hizo, bibi harusi huyo aliyetambulika kwa jina la Dasplang Rinset Lisa, ameamua kubadilisha tamaduni ya kuvalia gauni jeupe kwenye harusi na kuvaa gauni jeusi na alionekana kupendeza ndani yake.

Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Lisa alifichua kwamba watu wengi walimuuliza maswali mengi kuhusu kwa nini aliamua kuvaa nguo nyeusi siku ya harusi yake.

“Nilipata maswali mengi kuhusu kwa nini nilichagua kuvaa gauni jeusi kwenye harusi yangu. Sawa nina majibu mengi ya maswali, hili nitaandika baadaye, lakini kwa sasa kuna mtu yeyote anaweza kuniambia kwa nini atapendelea gauni jeupe na kwa nini asipende rangi nyingine yoyote ya mavazi?” alimaka.


This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

BIBI HARUSI AZUA GUMZO KUVAA SHELA YA RANGI NYEUSI KWENYE HARUSI YAKE

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×