Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

KOFFI OLOMIDE APIGWA STOP KUFANYA TAMASHA RWANDA



Wanaharakati wa haki za wanawake Nchini Rwanda wamelipiga ‘stop’ tamasha la mwamba wa Rhumba wa Congo, Koffi Olomide kwa tuhuma za ubakaji na unyanyasaji wa kingono anazokabiliwa nazo katika Mahakama za Ufaransa.


Mwezi Desemba, Mahakama ya Paris nchini Ufaransa itatoa uamuzi wa rufaa iliyoombwa kwa mashtaka dhidi ya Le Grand Mopao Mokonzi ambaye alipatikana na hatia ya kuwanyanyasa kijinsi wanenguaji wake wanne wa zamani.


Juliette Karitanyi, mwanaharakati mjini Kigali, Rwanda anasema kumruhusu Koffi Kutumbuiza Nchini Rwanda itakuwa ni kutoheshimu waathiriwa wa unyanyasaji wa kingono.


Hata hivyo, baadhi ya watetezi wa Mopao Mokonzi kwenye mitandao ya kijamii wanasema hakuna msingi wa kisheria wa kumzuia kutumbuiza nchini Rwanda.


This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

KOFFI OLOMIDE APIGWA STOP KUFANYA TAMASHA RWANDA

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×