Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Hukumu Kesi ya Lengai Ole Sabaya na Wenzake Kutolewa Leo


Mahakama  ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Arusha, leo inatarajia kutoa hukumu katika kesi ya jinai namba 105 ya unyang’anyi wa kutumia silaha inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, mkoani Kilimanjaro, Lengai Ole Sabaya (34).

Washtakiwa wengine katika shauri hilo ni Silvester Nyegu(26) na Daniel Mbura(38), ambao wanakabiliwa na mashtaka matatu ya unyang'anyi kwa kutumia silaha.

Kesi hiyo ilinguruma kwa siku 35 mfululizo mbele ya Hakimu Mwandamizi wa mahakama hiyo, Odira Amworo hadi kufikia tamati.

Upande wa Jamhuri ulikuwa na mashahidi 11 na vielelezo 10 vya ushahidi na viliwasilishwa mahakamani kama sehemu ya ushahidi.

Mashahidi wa upande wa utetezi, walikuwa watatu na walijitetea kwa njia ya kula kiapo na kuwasilisha baadhi ya nyaraka kama vilelezo vya ushahidi.





This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

Hukumu Kesi ya Lengai Ole Sabaya na Wenzake Kutolewa Leo

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×