Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

RAIS WA CHAD AUAWA KWA KUSHAMBULIWA NA WAASI


Jeshi la Chad limetangaza kuwa Rais wa Nchi Hiyo Idriss Deby amefariki baada ya kupata majeraha kwenye mapambano dhidi ya waasi.

Deby alienda mwishoni mwa wiki kuvitembelea vikosi vya nchi hiyo ambavyo vinapambana na waasi kaskazini mwa nchi hiyo. Waasi hao wamevuka mpaka wakitokea Libya.

Kifo chake kimetokea ikiwa ni saa chache tu tangu matokeo ya awali ya uchaguzi uliofanyika Aprili 11 kuonesha kuwa anaongoza kwa asilimia 80. Kwa ushindi huo, Deby angeiongoza nchi hiyo kwa awamu ya sita mfululizo.

Serikali na bunge vimevunjwa na sasa baraza la kijeshi ndilo litakaloiongoza nchi hiyo kwa kipindi cha miezi 18 ijayo.





This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

RAIS WA CHAD AUAWA KWA KUSHAMBULIWA NA WAASI

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×