Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

SIMBA SC YAICHAPA MWADUI FC 1 - 0 KAMBARAGE


 Bao pekee la Nahodha John Raphael Bocco leo limeipa Simba SC ushindi wa 1-0 dhidi ya wenyeji, Mwadui FC kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.
Bocco amefunga bao hilo dakika ya 66 kwa kichwa akimalizia mpira uliounganishwa kwa kichwa pia na beki Mkenya, Joash Onyango kufuatia kona ya winga Mghana, Bernard Morrison kutoka upande wa kulia.

Ushindi huo unawafanya Wekundu hao wa Msimbazi wafikishe pointi 52 baada ya kucheza mechi 22 na kurejea nafasi ya pili, sasa wakizidiwa pointi mbili na Yanga SC ambao hata hivyo wamecheza mechi tatu zaidi.


This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

SIMBA SC YAICHAPA MWADUI FC 1 - 0 KAMBARAGE

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×