Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

TUNDU LISSU KUTUA TANZANIA KESHO...KUTOA HESHIMA ZA MWISHO KWA RAIS MSTAAFU BENJAMIN MKAPA



Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimesema kuwa kesho Jumatatu Julai 27,2020 Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Tundu Lissu atarejea nyumbani nchini Tanzania na kesho kutwa Julai 28,2020 atahudhuria shughuli za utoaji wa heshima za mwisho Kwa Rais Mstaafu Benjamin William Mkapa, katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.

Taarifa hiyo imetolewa leo Julai 26, 2020, na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa chama hicho Tumaini Makene.

Amesema Tundu Lissu anatarajiwa kuwasili nchini Tanzania Siku ya Jumatatu Julai 27,2020 majira ya saa saba na dakika 20 mchana ambapo atatua katika ardhi ya Tanzania kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) akisafiri na shirika la ndege la Ethiopia (Ethiopian Airlines) kutokea Ubelgiji.

Aidha Makene amesema siku ya Jumanne Julai 28,2020 , Tundu Lissu atahudhuria shughuli ya utoaji wa heshima za Mwisho Kwa Rais Mstaafu Hayati Benjamin William Mkapa katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es salaam na kwamba ratiba ya shughuli zingine zitatolewa.
SOMA ZAIDI >
Via EATV


This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

TUNDU LISSU KUTUA TANZANIA KESHO...KUTOA HESHIMA ZA MWISHO KWA RAIS MSTAAFU BENJAMIN MKAPA

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×