Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Kesi ya Tundu Lissu Yakwama Tena

Kesi inayomkabili aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na wenzake imeshindwa kuendelea baada ya Upande wa Mashtaka kushindwa kuwasilisha jalada la Kesi hiyo

Mahakama hiyo jana ilitarajia kusikiliza maombi yaliyowasilishwa na wadhamini wa mshitakiwa huyo wakiomba mahakama kutoa hati ya kumkamata mshitakiwa huyo kwa kuwa wao wameshindwa.

Wakili wa Serikali, Ester Martin alimueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba kuwa mwendesha mashitaka anayesikiliza shauri hilo hayupo hivyo anaomba mahakama hiyo kupanga tarehe nyingine kwa ajili ya kusikilizwa.

Baada ya Upande wa mashitaka kuwasilisha hoja hiyo, Hakimu Simba ameahirisha kesi hiyo hadi Aprili 23, 2020 kwa sababu ya Upande wa Mashitka umeshindwa kuwasilisha jalada la kesi hiyo mahakamani hapo.




This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

Kesi ya Tundu Lissu Yakwama Tena

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×