Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Infinix Kuipamba Valentine Kwa Uzinduzi Duka La Pili La Kisasa-Infinix Smart Hub.

Katika Kusheherekea sikukuu ya wapendanao, kampuni ya Simu, Infinix Mobile Tanzania imezindua rasmi duka Jipya, maarufu kama Infinix Smart Hub, lililopo China Plaza Kariakoo. Hili ni duka la pili la kuzinduliwa na kampuni hiyo huku lengo kuu ni kuwafikia wateja wake kwa urahisi zaidi.

Katika uzinduzi huo afisa wa mahusiano wa kampuni ya simu ya Infinix, Aisha Karupa alivieleza vyombo vya habari kuwa, “Infinix imejipanga vizuri katika kutoa huduma iliyo bora zaidi kwa wateja wetu wa maeneo mbalimbali pasipo kuwa na hofu ya kutufikia kwa uharaka zaidi na katika kuhakikisha tunafanikiwa katika hilo Infinix Smart Hub itakuwa ikitoa huduma kwa siku saba za kila wiki yani jumatatu hadi jumapili kuanzia saa 9:00 asubuhi hadi saa 11:30 jion”.
 
Aisha aliwashukuru watanzania kwa kuzipokea bidhaa za Infinix na kuwa wateja wazuri kwao, kusema “kwa mapenzi yenu tutaendelea kutanua wigo ili kuhakikisha mnapata huduma stahiki kama vile simu na bidhaa nyingine za Infinix zenye ubora zaidi zikiwa chini ya warranty ya mwaka mmoja na mwezi moja pamoja na elimu ya bure kuhusiana na utunzaji na utumiaji wa simu za Infinix kwa muda mrefu pasipo kuwaletea shida ya aina yoyote”. 
 
Vile vile Meneja wa Masoko Bwana Saiphone Asajile alieleza machache kuhusiana na mauzo ya Infinix tangu kuingia kwake rasmi Tanzania mwaka 2018 na ni nini watanzania wategemee kutoka Infinix hasa kwa kipindi hiki cha valentine,
“Watanzania wameonyesha upendo wa hali ya juu sana kwetu na hadi kufikia hatua ya kuzindua duka la pili la kisasa sio hatua ndogo, kwani kuna kampuni nyingi za simu tumezikuta lakini hawajafanikiwa kufanya hili tunalolifanya Infinix, hiki ni kiashirio tosha Infinix imeliteka soko la simu kwa asilimia kubwa lakini vile vile katika kuendeleza upendo kama ilivyo kawaida yetu katika Msimu huu wa Valentine Infinix inakupa ofa ya 10%, Infinix gift package na chakula cha usiku kwa wewe na umpendaye katika restaurant ya kisasa”.
 
Uzinduzi huo ulishamirishwa na michezo mbalimbali pamoja na muziki wa live band na kuufanye uwe wa kipekee.





This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

Infinix Kuipamba Valentine Kwa Uzinduzi Duka La Pili La Kisasa-Infinix Smart Hub.

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×