Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

BABU AVAMIA BENKI NA KUIBA PESA NA KUZIGAWA KAMA ZAWADI AKISEMA 'MERRY CHISTMAS'

Bwana mmoja mwenye ndevu nyeupe amefanya uvamizi wa Benki siku mbili kabla ya Krismasi na kuzirusha juu kwa furaha na kuwatakia kheri ya sikukuu wapita njia, mashuhuda wameeleza.

Polisi wamethibitisha "mwanaume mzee wa kizungu" alivamia benki ya Academy mjini Colorado Springs, Marekani siku ya Jumatatu.

"Aliiba pesa benki, akatoka nje na kuzitawanya kwa watu," shuhuda Dion Pascale alikiambia kituo cha Colorado's 11 News.

"Alianza kurusha fedha kutoka kwenye begi na kisha akaanza kusema, 'Merry Christmas!'"

Kwa mujibu wa mashuhuda, Mtuhumiwa Huyo akapiga hatua chache kutoka benki na kuketi mbele ya mkahawa wa Starbucks akisubiri kukamatwa.

Katika hali ambayo inaweza kuwa ya kustaajabisha kwa wakazi wa Afrika Mashariki, wapita njia wanaripotiwa kuwa walichota fedha zote zilizozagaa na kuzirudisha benki.

Polisi wamemtaja mtuhumiwa huyo kwa jina la David Wayne Oliver, mwenye miaka 65.

Polisi hawadhani kuwa alikuwa na usaidizi wowote.
Chanzo - BBC


This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

BABU AVAMIA BENKI NA KUIBA PESA NA KUZIGAWA KAMA ZAWADI AKISEMA 'MERRY CHISTMAS'

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×