Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

BIDHAA ZILIZOISHA MUDA WA MATUMIZI,ZILIZOBADILISHWA LEBO ZAKAMATWA KWENYE MADUKA SHINYANGA MJINI

Kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Shinyanga ikishirikiana na wakaguzi kutoka shirika la viwango TBS imefanikiwa kukamata shehena ya Bidhaa Zilizoisha Muda wa zikiendelea kuuzwa katika maduka makubwa maarufu kama Supermarket mjini Shinyanga.

Bidhaa hizo zimekamatwa jana kutokana na msako katika maduka mbalimbali Mjini Shinyanga na kukamata shehena ya bidhaa mbalimbali ikiwemo chakula na vipodozi ambazo zimeisha muda wa kutumika vikiendelea kuuzwa madukani.

Akizungumza baada ya kufanya ukaguzi huo,Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa Mhe. Jasinta Mboneko ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Shinyanga amesema licha bidhaa nyingi madukani kuwa zimeisha muda wa kutumika pia wamebaini kuna udanganyifu mkubwa wa kubadilisha lebo za muda wa matumizi katika bidhaa mbalimbali ili ziendelee kuuzwa sokoni.

Naye Mkaguzi wa kutoka Shirika la Viwango Tanzania TBS Helen Andrew amesema operesheni hiyo sasa ni endelevu kwa mikoa yote.
Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa Mhe. Jasinta Mboneko akiangalia bidhaa ndani ya duka


This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

BIDHAA ZILIZOISHA MUDA WA MATUMIZI,ZILIZOBADILISHWA LEBO ZAKAMATWA KWENYE MADUKA SHINYANGA MJINI

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×