Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Matumaini ya Kupatikana Dawa ya Kutibu Ugonjwa wa Ebola Yaanza Kuonekana

Wizara ya Afya katika jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo imesema Dawa mbili za majaribio ya kuutibu ugonjwa wa Ebola zinaonekana kuyanusuru maisha ya wagonjwa. 

Dawa hizo zinazotokana na kingamwili ,za watu walionusurika na ugonjwa huo hatari zimeonyesha mafanikio mema miongoni mwa wagonjwa waliozitumia, katika juhudi za kupambana na mripuko wa sasa wa Ebola Mashariki mwa Kongo. 

Aina nne za dawa zilikuwa zikifanyiwa majaribio, lakini aina mbili, REGN-EB3 na mAb114 zilionekana kuleta tija. Mbili nyengine, ZMapp na Remdesivir sasa imeamuliwa zisitumiwe. 

Mkurugenzi wa Taasisi ya Kimarekani kwa ajili ya magonjwa ya kuambukiza Antony Fauci amesema mafanikio ya dawa hizo ni habari njema, ambazo zinaashiria kupatikana tiba dhidi ya maradhi ambayo katika kipindi cha hivi karibuni hakuna aliyekuwa akifikiria. 

Shirika la Afya Ulimwenguni WHO limewahimiza wagonjwa wa Ebola kutafuta dawa hizo haraka.




This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

Matumaini ya Kupatikana Dawa ya Kutibu Ugonjwa wa Ebola Yaanza Kuonekana

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×