Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakari bin Zuberi Atoa Pole Kwa Wafiwa na Majeruhi Ajali ya Moto Morogoro

Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakari Bin Zuberi ametoa salamu za pole kwa Rais, wafiwa na wote walioguswa na msiba kufuatia ajali ya moto mkoani Morogoro na kuagiza BAKWATA mkoa wa Morogoro kutoa ushirikiano wote utakaohitajika katika kipindi hiki.

Ajali hiyo imetokea jana Jumamosi Agosti 10, 2019   baada ya lori la mafuta kupinduka na kuwaka moto muda mfupi baada ya watu kuanza kuchota mafuta hayo.

Wakati huohuo, Sheikh Abubakari bin Zuberi  amesema swala ya sikukuu ya Eid Agosti 12,kitaifa itaswaliwa katika kiwanja cha Masjid Kibadeni Chanika ikifuatiwa na baraza la Eid na mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri wa TAMISEMI Selemani Jafo.




This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakari bin Zuberi Atoa Pole Kwa Wafiwa na Majeruhi Ajali ya Moto Morogoro

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×