Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

IGP SIRRO AWATOA HOFU WANANCHI TISHIO LA SHAMBULIZI LA KIGAIDI


Jeshi la Polisi Nchini Tanzania limewatoa hofu wananchi juu ya tishio la ugaidi katika maeneo ya Masaki jijini Dar es Salaam, likisema taarifa hizo zimeshaanza kufanyiwa kazi.

Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) nchini Tanzania, Simon Sirro amesema kuwa jeshi lake lilishapata fununu za shambulio hilo kabla Ubalozi wa Marekani kutoa tahadhari juu ya tukio hilo kupitia tovuti yake Juni 18, 2019.

Akizungumzia taarifa hiyo ya Ubalozi wa Marekani Nchini Tanzania, IGP Sirro amesema, “hiyo ni taarifa kama taarifa nyingine, inaweza kuwa ya kweli au uongo, lakini sisi kama vyombo vya ulinzi huwa hatupuuzi jambo. Tangu  Jumanne Juni 17, 2019 tulipata hiyo taarifa kwa hiyo tuko vizuri, timu zetu za operesheni na intelijensia na wengine tunaifanyia kazi.”

Katika tangazo lake Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania inaeleza kuwapo kwa uvumi wa kutokea kwa shambulio la kigaidi katika eneo la Masaki hususan hoteli za kitalii na maduka ya maeneo hayo ya ufukwe wa Bahari ya Hindi.

Ubalozi huo umewataka wakazi kuwa makini na maeneo hayo, kujiepusha na makundi na kufuatilia taarifa kupitia vyombo vya habari.




This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

IGP SIRRO AWATOA HOFU WANANCHI TISHIO LA SHAMBULIZI LA KIGAIDI

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×