Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Waziri Mkuu Uingereza May ajiuzulu rasmi wadhifa wake

Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May ameachia uongozi wa chama tawala cha Conservative hii leo hatua inayofungua mlango wa kinyang'anyiro cha mrithi wa nafasi hiyo. 

May hatauhutubia umma lakini amewasilisha barua ya kuthibitisha kujiuzulu kwake kwa kamati ya chama chake yenye nguvu ijulikanayo kama "Kamati ya 1922".

 May ataendelea kuwa waziri mkuu hadi wabunge watakapomchagua kiongozi mpya wa chama hicho mchakato utakaouchukua hadi miezi miwili. 

Waziri wa zamani wa mambo ya nje Boris Johnson anapewa nafasi kubwa ya kushinda nafasi hiyo. 

Waziri Mkuu May alitangaza kujiuzulu nafasi hiyo Mei 24 baada ya kushindwa kufanikisha makubaliano ya Uingereza kujiondoa Umoja wa Ulaya ama Brexit.




This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

Waziri Mkuu Uingereza May ajiuzulu rasmi wadhifa wake

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×