Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

BINTI AUNGUZWA MAJI YA MOTO BUKOBA


Mwanafunzi aliyeunguzwa Maji ya moto

Binti wa darasa la saba, shule ya msingi Kashenge katika Manispaa ya Bukoba, amelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera akiuguza majeraha anayodai kuyapata baada ya kuunguzwa kwa maji ya moto na mama yake wa kambo.

Akizungumza kwa shida akiwa wodini, Binti Huyo mwenye umri wa miaka 16, Amesema Kuwa alimwagiwa maji ya moto na mama huyo kwa sababu alipika viazi bila kuambiwa.

Afisa Muuguzi Msaidizi wa wodi namba kumi upande wa upasuaji, Edith Ezekiel amesema kuwa walimpokea binti huyo jana akiwa ameunguzwa mkono wa kulia, titi na sehemu za bega, na kuwa hali yake kwa sasa sio mbaya na anaendelea na matibabu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Revocatus Malimi amesema kuwa atatoa taarifa rasmi kesho kuzungumzia tukio hilo ambalo tayari limeripotiwa polisi na kufunguliwa jalada la kujeruhi namba RB/2466/19.


This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

BINTI AUNGUZWA MAJI YA MOTO BUKOBA

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×