Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

NIGERIA WATAMBA KUITWANGA SERENGETI BOYS MCHEZO WA UFUNGUZI KESHO

Kocha Manu Garba wa timu ya Taifa Nigeria chini ya miaka 17, amesema hana presha na Mchezo Wao wa ufunguzi dhidi ya Tanzania.

Amesema anaifahamu Tanzania vizuri baada ya kukutana nao katika Mashindano ya Uefa Assist nchini Uturuki hivyo ana imani mchezo Wao Utakuwa Mzuri. "Tanzania ni vijana wadogo na wanacheza mpira wa pasi nyingi, wanacheza kwa kuelewana na sio timu ya kawaida," alisema.

Ameongeza Mchezo Wao Utakuwa mzuri kwa timu zote kuhitaji matokeo mazuri uwanjani ili kuanza vizuri Fainali hizo.

Wakati huohuo nahodha wa Nigeria, Tijani Samson amesema wamejiandaa vizuri kuweza kupata matokeo katika mchezo huo bila kuwa na wasiwasi wowote.

Na Thomas Ng'itu - Mwanaspoti


This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

NIGERIA WATAMBA KUITWANGA SERENGETI BOYS MCHEZO WA UFUNGUZI KESHO

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×