JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
| | | OFISI YA RAIS |
Anuani ya Simu: “TAMISEMI” | Tawala za MKOA na | ||
Simu Na: (026) 2322848, 2321607 | Serikali za Mitaa, | ||
2322853, 2322420 | Jengo la Mkapa, | ||
Nukushi: (026) 2322116, 2322146 | 2 Barabara ya hospitali, | ||
2321013 | | S.L.P. 1923, | |
Barua pepe: [email protected] | 41185 DODOMA. | ||
| | | |
Unapojibu tafadhali taja: | | ||
Kumb. Na. CD. 162/355/01 | 30 Oktoba, 2017 |
TANGAZO LA KUITWA KAZINI
OR TAMISEMI kwa kushirikiana na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inapenda kuwataarifu waombaji kazi wa nafasi mbalimbali za kada za Afya walioomba kazi kuanzia tarehe 25/07/2017hadi tarehe 30/08/2017 kuwa mchakato wa kuwapangia vituo vya kazi umekamilika.
Aidha, mnatakiwa kuripoti katika vituo vya kazi mlivyopangiwa katika muda wa siku kumi na nne (14) kuanzia tarehe ya tangazo hili mkiwa na vyeti halisi (Originals Certificates) vya masomo kuanzia kidato cha nne na kuendelea kwa ajili ya kuhakikiwa na mwajiri kabla ya kupewa barua ya ajira.
Orodha ya majina ya waliopangiwa vituo vya kazi inapatikana kupitia tovuti ya OR TAMISEMI www.tamisemi.go.tz. Hakutakuwa na mabadiliko ya vituo, watakaoshindwa kuripoti katika muda uliopangwa, nafasi zao zitajazwa na waombaji wengine wa kada husika.
Kwa wale ambao majina yao hayakuonekana katika tangazo hili watambue kuwa hawakupata nafasi hivyo wasisite kuomba kwa mara nyingine nafasi za kazi zitakapotangazwa. Nafasi za Wauguzi na Wahudumu wa Afya zitatangazwa mara baada ya kukamilisha zoezi la uchambuzi na uhakiki wa vyeti.
Waajiri wote mnaelekezwa kuwapokea, kuhakiki vyeti na kuwafanyia mafunzo elekezi (Induction Course) kabla ya kuwapangia vituo vya kazi.
Limetolewa na:-
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
OR – TAMISEMI
30/10/2017
KUYAONA MAJINA HAYO
>>>BONYEZA HAPA--PDF