Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

NAWATAKIA HERI YA MWAKA MPYA

 
Kitendo cha kuendelea kupumua na kufanikiwa kuuona Mwaka mpya 2018 unapaswa kushukuru, mshukuru Mungu bila kuangalia una hali gani ama yale uliyoyapa kuwa kwa mwaka 2017 hayajawa..
Binafsi nimeshashukuru na nachukua nafasi hii kukutakia kila la heri katika mwaka huu mpya wa 2018, ni wazi utakuwa mwaka wa kumalizia pale ulipoishia muda ambao mimi nalitazamia hilo kwako bila kuficha hicho ndicho nitakachokifanya kwangu/kwetu.. Yapo ambayo niliyapanga kwa mwaka 2017 yawe yametimia lakini kwa mapenzi ya mungu hayajatia hivyo imani na juhudi zetu mwaka huu yaweze kuwa....
Hii ni nafasi nzuri kwako kukushukuru wewe ambae kila leo unapita kwenye hii blog na kupatamawili matatu, nakushukuru sana kwakuwa bila wewe hata hii blog isingefika hapa, muda ambao wewe unapata faida kupitia hii blog kwa upande wangu pia nimepata faidi kupia hii blog.. 
Awali sikuwa najua kama naifikia idadi kubwa ya jamii ila pongezi na maoni nnayoyapa ndio yaliyopelekea niwe serious zaidi.. Kama ambavyo wengine wanaamini ya kuwa kwenye blog hii ndio sehemu pekee ambayo utapata kujua kiundani kuhusu ving'amuzi vyote, na ulimwengu mzima waDigital tv bila kuvutia biashara, nawe unapaswa kuamini hivyo lengo la blog hii ni kukupa wewe ELIMU, USHAURI,MSAADA, HUDUMA na HABARI kuhusu yote yanayohusu ulimwengu wa Digital tv, mlionufaika na blog hii mtakuwa mpo pamoja nami kwa msemo wangu huu.
Moja ambalo binafsi linaenda kunikwaza ni jinsi ya unavyohitaji msaada, wachache wenu hamzingatii muda, mimi sifanyi mazungumzo na mdau yeyote kwa saa 24 isipokuwa ni kuanzia saa 2 asubuhi mapaka saa 2 usiku kila siku na huwa sina utaratibu wa kuzima simu, kutokuwa na utaratibu wa kuzima simu imekuwa ndio fimbo ya kunipigia.. Nilishawahi kupokea simu alfajiri mdau ana shida.. saa 6 usiku.. saa 8 usiku... saa4 ama 5 usiku ndio nyingi sana..
Huwa napokea kwakuwa hii namba sio ya wadau wa humu tu hata wale watu wangu wengine ila nnapogundua ni wadau wangu nawaomba wapige muda wa kazi. Naomba nisisitize simu ya humu haifanyi kazi saa 24 hivyo kabla ya saa 2 asubuhi usipige na baada ya saa 2 usipige.
Mungu ibariki Tanzania!



This post first appeared on Mustapha MaDish Tech, please read the originial post: here

Share the post

NAWATAKIA HERI YA MWAKA MPYA

×

Subscribe to Mustapha Madish Tech

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×