Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Exim yachangia milioni 25/- ununuzi vitanda sekondari

Na MWANDISHI WETU -ARUSHA

BENKI ya Exim Tanzania imechangia Sh milioni 25 kwa ununuzi wa vitanda pacha 47 vya hosteli ya wanafunzi wa Shule mpya ya Sekondari Mrisho Gambo iliyopo mkoani Arusha. 

Hatua hiyo ni mwendelezo wa benki hiyo kuunga mkono jitihada za Serikali katika kuboresha sekta ya elimu nchini.

Akizungumza jana jijini hapa, wakati wa hafla ya kukabidhi msaada huo iliyoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Exim Tanzania, Jaffari Matundu alisema mchango huo ni sehemu ya mpango wa uwajibikaji kwa jamii (CSR) unaotekelezwa na benki hiyo ukifahamika kwa jina la Exim Cares, ukilenga kusaidia jamii.

“Benki ya Exim tunaamini kuwa tunalo jukumu kubwa la kufanya katika kuwezesha mabadiliko chanya katika jamii zinazotuzunguka. 

“Elimu ni kati ya maeneo yetu ya kuzingatia na mpango huu unaendana na mkakati wetu wa kubadilisha maisha ya wanafunzi chini ya mpango wa Exim Cares kupitia vitendo endelevu.

“Benki ya Exim tunavutiwa zaidi katika kuleta athari chanya kwenye jamii ambazo tunatoa huduma zetu, hivyo kwa kuangalia nafasi yetu tumeona kwamba kwenye hili tunaweza kusaidia vitanda pacha vipatavyo 47 vikiwa na uwezo wa kubeba wanafunzi zaidi ya 100,” alisema Matundu.

Alitoa wito kwa taasisi na wadau mbalimbali nchini kuhakikisha wanawekeza kwenye uwezeshaji wa vijana kupitia elimu kutokana na ukweli kuwa bado wanakabiliwa na changamoto nyingi.

Alipongeza Serikali kwa kutoa elimu ya msingi bure kwa watoto wote, hatua ambayo imekuwa ni msaada mkubwa kwa watoto wanaopitia changamoto mbalimbali za kiuchumi wakiwamo yatima, wenye mahitaji maalumu ya kielimu pamoja na vikundi vingine vyenye vya watoto wanaoishi mazingira magumu.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Gambo, aliipongeza benki hiyo kwa msaada huo, huku akibainisha kuwa umetolewa kwa wakati mwafaka.

“Kupitia msaada huu kutoka Benki ya Exim tutaweza kuwasaidia wanafunzi wetu kukaa hosteli, hasa wale ambao kwa sasa wanatembea umbali mrefu kwenda na kurudi. 

“Kwa kweli kupitia msaada huu utawawezesha kujifunza vizuri na kutambua ndoto zao za masomo,” alisema Gambo.

Alisema kuwa mahitaji ya mradi huo ni vitanda 100 na magodoro ambavyo vitagharimu Sh milioni 53.7.

Source: mtanzania.co.tz

The post Exim Yachangia Milioni 25/- ununuzi vitanda sekondari appeared first on News Africa Now.



This post first appeared on News - News Africa Now, please read the originial post: here

Share the post

Exim yachangia milioni 25/- ununuzi vitanda sekondari

×

Subscribe to News - News Africa Now

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×