Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Mwalimu Atiwa Mbaroni Kwa Kumwazibu Mwanafunzi

Jeshi la Polisi mkoani Tanga linamshikilia Mwalimu wa Shule ya Sekondari Mkwakwani kwa kumpiga na kumsababishia madhara ya kiafya mwanafunzi, Suleyman Mohamed (18).
Mwanafunzi huyo inadaiwa alichapwa viboko juzi asubuhi na mwalimu huyo wa zamu aliyekuwa akiwaadhibu wanafunzi waliochelewa na waliokuwa wakipiga kelele darasani.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Benedict Wakulyamba amesema tayari mwalimu huyo yuko mikononi mwa jeshi hilo na upelelezi wa suala hilo unaendelea.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Thobias Mwilapwa amewataka walimu kuwa waangalifu wakati wakiwaadhibu wanafunzi ili kukwepa madhara kwa wanafunzi.
“Tunalifuatilia kwa karibu tukio hili. Niseme kwamba tutachukua hatua stahiki ikithibitika kuwa umefanyika uzembe,” amesema Mwilapwa.
Baada ya kuchwapwa, mwanafunzi huyo amelazwa katika Hospitali ya Rufani ya Bombo ikielezwa kwamba tayari amepatiwa rufaa kuhamishiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya matibabu zaidi.



This post first appeared on HABARI ZA SIASA NA MUZIKI, please read the originial post: here

Share the post

Mwalimu Atiwa Mbaroni Kwa Kumwazibu Mwanafunzi

×

Subscribe to Habari Za Siasa Na Muziki

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×