Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Blagnon amerudi Simba baada ya kukwama uarabuni

UNAMKUMBUKA yule Mshambuliaji mwenye thamani ya shilingi milioni 100 kutoka Ivory Coast Fredirick Blagnon? Amerejea tena Simba SC Kwa sababu ya Itc Yake Kuwa na matatizo na kushidwa kukamilisha uhamisho wa mkopo kujiunga na Oman Club ya Oman.
Blagnon alitolewa Kwa Mkopo na Simba mwezi wa kwanza ila kutokana na ITC yake kuwa na Matatizo na kushidwa kuituma kwa wakati Club ya OMAN imeamua kusitisha usajili huo wa mkopo.
Shaffidauda.co.tz imezungumza na Makamu Mwenyekiti wa Simba Godffrey Nyange ‘Kaburu’ ambaye amethibitisha kumpokea Blagnon jana usiku na leo ameanza safari ya kwenda Arusha kuungana na timu.
Simba inaelekea mkoani Arusha kucheza mchezo wao robo fainali wa ASFC dhidi ya Madini FC utakaochezwa Jumapili hii Machi 19.



This post first appeared on HABARI ZA SIASA NA MUZIKI, please read the originial post: here

Share the post

Blagnon amerudi Simba baada ya kukwama uarabuni

×

Subscribe to Habari Za Siasa Na Muziki

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×