Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

JANGA LA UNENE KUPITA KIASI


Tatizo la unene uliokithiri limeongezeka sana kiasi kwamba wataalamu wa afya wameanza kuliita gonjwa la mlipuko.  Ugonjwa wowote ukizidi katika jamii au eneo fulani, sayansi ya tiba huliita janga, lakini ikitokea katika sehemu nyingi za ulimwengu kwa wakati mmoja pia huliita janga.

Kulingana na shirika la afya ulimwenguni, kwa uchache watu milioni 2.8 hufa duniani kote kila mwaka kwa sababu ya kunenepa kupita kiasi.  Tatizo hili lipo katika nchi tajiri na maskini pia.  Unene Kupita Kiasi si suala la jamii zenye kipato kikubwa tena.

Unaweza kukokotoa kiwango cha unene, ambao huelezewa kama usio wa “mrundikano mkubwa au uliokithiri wa shahamu unaoweza kudhuru afya,” kwa kutafuta kiashirio cha Uzito wa mwili wako (Body mass index [BMI]).  Kufanya hesabu hiyo, gawa uzito wako katika paundi kwa kipeo cha pili cha urefu wako katika inch kisha zidisha kwa 703.  BMI yako 25 au zaidi, una uzito mkubwa, na kama ni 30 au zaidi, una ugonjwa wa kunenepa kupita kiasi.  Kwa hali zote mbili, ni vyema kuanza program ya kubadili mtindo wa maisha.

Kwa kifupi fomyula katika vipimo vya metriki ni: BMI = (uzito katika kilo) / (urefu katika mita x uzito katika mita).  Kwa mfano, kama uzito wako ni kilo 60 na una urefu wa mita 1.70, BMI itakuwa BMI =60 / (1.7 x 1.7) = 20.8 (upo katika kategoria ya kawaida).

Kama hutaki kuhangaika na mahesabu, ingia tu katika intaneti upate kikokotoo cha BMI.  Utapata vingi, vya vipimo vya kiingereza na vya metriki.

BMI inaashiria nini?  Je, uko hatarini?  Je, una uzito mkubwa?  Shinikizo la damu yako ni la kawaida?  Je, unakula mafuta mengi, karoli, au vyakula vilivyokobolewa na kusindikwa?  Je, chakula chako cha kawaida hutoka katika migahawa ya chakula cha haraka?  Kama ni hivyo, uko hatarini, au tayari unaweza kuwa na matatizo ya kiafya na hujui.

Vyombo vya habari hutangaza njia nyingi “za ajabu” za kupunguza uzito, lakini njia bora kuliko zote ni badiliko kubwa la mtindo wa maisha.


This post first appeared on Afya Na Kiasi, please read the originial post: here

Share the post

JANGA LA UNENE KUPITA KIASI

×

Subscribe to Afya Na Kiasi

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×