Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

UKIZIDISHA DAWA YANATOKEA HAYA


Unapougua maana yake kinga zako za Mwili zimeelemewa na vijidudu vya maradhi vilivyoingia mwilini.  Licha ya kuelemewa huko, mfumo wa kinga unayo namna ya kujibadili na kukabiliana vyema.

Endapo adui atakuwa mkubwa au mgonjwa anataka kupona haraka, Dawa huhitajika ili kuziongezea nguvu.  Dawa hizi, zisipotumika vizuri hasa zikizidishwa, huweza kusababisha kifo.

Miili yetu imeundwa kwa chembe ndogondogo zinazoitwa seli ambazo hutengeneza viungo vyote vya mwili kama vile moyo, ubongo, ini, figo, ngozi, mapafu na ngozi.

Kufanikisha chochote, miili hufanya kazi kwa kutegemea kemikali mbalimbali kama vile protini, vichocheo vya kikemikali, vitamin au madini ambazo husaidia kuuambia mwili ufanye nini au ufanyeje kazi.

Seli za mwili pia husaidia kuhamisha taarifa na kuusaidia kufanya kazi azitakazo mhusika kama kawaida.  Shughuli hizi zote hufanywa na homoni pamoja na vichocheo vinavyoundwa na seli.
Ili mwili ufanye kazi vizuri na maisha yaendelee ni lazima kusiwe na kitu ambacho kinaingilia na kuingilia ufanisi wa seli na kemikali mbalimbali zinazoratibu maisha na afya ya mwili.

Mtu akimeza Kiasi Kikubwa Cha dawa ambazo, ikumbukwe, zote ni kemikali, anakuwa amezidisha uwezo wa mwili kuzidhibiti kemikali hizo, hivyo seli za mwili huathirika, kudhoofu hata kufa.
Dawa pia huweza kuingilia utendaji kazi wa kemikali za mwili hatimaye kusababisha mgonjwa kupoteza maisha.

Inategemea kiasi cha dawa ambacho mtu amezidisha.  Ikiwa ni kiasi kidogo basi mwili utazidiwa kwa muda, baadhi ya seli zitakufa na ufanyaji kazi wa viungo utaathirika kidogo.  Madhara ya kiasi kidogo cha dawa yanaweza kumalizwa hospitalini.

Endapo mtu atazidisha kiasi kikubwa cha dawa basi seli nyingi zaidi za viungo vya mwili vitaathirika.  Kwanza, seli zitakufa na viungo vitashindwa kufanya kazi.  Mfano wa kiungo muhimu kinachoathirika na kuweza kuhatarisha maisha ni ini.  Endapo kazi zote za ini zitasimama na hali ikaendelea kuwa hivyo kwa muda, basi mhusika anaweza kupoteza maisha.

Kingine kinachoweza kutokea baada ya kuzidisha kiasi kikubwa cha dawa kuzizuia seli na viungo husika.  Hili likidumu kwa muda mrefu, mgonjwa anaweza kupoteza maisha.  Mfano wa viungo vinavyoathiriwa sana ni figo, ubongo, moyo na mapafu.

Kuzidisha dawa za kupunguza au kuongeza presha, mapigo ya moyo au kisukari husababisha kushuka au kuongezeka zaidi kwa presha, mapigo ya moyo au kisukari na kusababisha kupasuka kwa mishipa ya damu kwa dawa za kuongeza presha.

Madhara mengine ya kuzidisha dawa hizi ni damu kuvujia mwilini jambo ambalo ni hatari zaidi kwani inaweza kwenda kwenye ubongo na kusababisha kiharusi, mapigo ya moyo kwenda kasi au kupungua zaidi, sukari kuzidi au kupungua sana.

Likitokea lolote kati ya hayo yaliyoelezwa huweza kusababisha kushindwa kwa viungo muhimu vya mwili na kuleta madhara makubwa.

Paracetamol au Panadol huweza kuharibu ini ndio maana mtu anashauriwa asimeze zaidi ya vidonge vinane kwa siku.  Ini likifa, maisha ya mgonjwa huwa hatarini.  Digoxin, dawa inayosaidia kuongeza nguvu ya moyo ikizidishwa huweza kuufanya moyo kusinyaa na kudunda kwa nguvu zaidi, moyo kushindwa kufanya kazi hatimaye kifo.

Dawa nyinginezo kama vile aspirin, diclofenac, meloxicam au piroxicam zinazosaidia kupunguza maumivu mwilini huweza kusababisha kufeli kwa figo hatimaye mwili hushindwa kufanya kazi vizuri na ikiendelea mwili huzidiwa na hatimaye kifo.


This post first appeared on Afya Na Kiasi, please read the originial post: here

Share the post

UKIZIDISHA DAWA YANATOKEA HAYA

×

Subscribe to Afya Na Kiasi

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×