Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

SABABU ZA KUJAA KWA TUMBO


Kila mmoja amewahi kuhisi tumbo kujaa wakati wote, hali hii hutokea mara kadhaa kwa nyakati tofauti.  Japo ni hali ambayo kwa kawaida inatokana na ulaji kupita kiasi, lakini kuna baadhi pia hawana tabia ya kula kupita kiasi bado wanakumbana na hali hiyo.

Hivyo ni vyema tukafahamu kuwa, sambamba na tabia za ulaji, kuna sababu zingine zinazochangia hali hii kama vile Mwili Kuhifadhi Kiwango kikubwa cha maji.

Pia inaweza kutokana na matatizo mengine ya kiafya kama vile dalili ya vidonda vya tumbo ambayo huambatana na uwepo wa gesi tumboni na hivyo kuongeza ujazo wa tumbo na matatizo mengine yanayojitokeza kwenye mfumo wa chakula.

Zifuatazo ni sababu nyingine zinazochangia kwa kiasi kikubwa sana kujaza tumbo na kusababisha kero kwa walio wengi.

“Premenstrual syndrome” hili ni jina la kitaalam linalotafsiri baadhi ya matatizo ya kiafya madogo kama vile uchovu, maumivu na hata kichefuchefu yanayojitokeza kwa mwanamke wakati akikaribia kuingia kwenye mzunguko wa hedhi.

Premenstrual syndrome pia inasababisha mwili kuhifadhi Kiwango Kikubwa Cha maji kutokana na mabadiliko ya mfumo wa homoni kwa wakati huo.

Hivyo, ndani ya kipindi, ni kawaida kwa mwanamke kuhisi tumbo lake limejaa wakati mwingi.

Ulaji wa chumvi kwa wingi ni moja ya sababu hizi.  Ni dhahiri kuwa miili yetu inahitaji chumvi, lakini mara nyingi tumejikuta tukitumia zaidi kiwango stahiki kinachostahili kuingia mwilini.

Chumvi ikizidi mwilini inaupa mfumo wa mwili Kuhifadhi Kiwango Kikubwa cha maji na chumvi pia inaweza kusababisha matatizo mengine makubwa ya kiafya kama vile shinikizo la juu la damu.

Kwa siku za karibuni, matumizi ya vyakula vilivyosindikwa yameongezeka maradufu, ni muhimu kuzingatia kuwa asilimia kubwa ya vyakula vilivyosindikwa vimewekwa kiasi kikubwa cha chumvi na hata kama usipohisi ladha ya chumvi kwenye vyakula hivyo haina maana kuwa havijawekewa chumvi.

Unywaji wa soda na vinywaji vingine vya kiwandani pia unachangia sana kulifanya tumbo muda wote liwe limejaa kama soda na vinywaji vingine kama bia, shampeni na vingine vyenye gesi.

Unapokunywa moja ya vinywaji hivi vinaenda kuongeza ujazo kwenye mfumo wako wa chakula.  Wakati ukiendelea kunywa, unaweza kutoa kiasi kidogo cha gesi, wengi wamezoea kuita kudukua au kubeua.  Hii inatokea pale unapokunywa kinywaji chenye gesi na ghafla inakujia hali kama unacheua hivi, lakini kinachotoka ni gesi.

Hii haimaanishi kuwa kwa kufanya hivyo, gesi yote uliyoipata kutoka kwenye kile kinywaji imetoka, hapana.  Kiasi kikubwa cha gesi hiyo huendelea kubakia kwenye utumbo wa chakula.

Ikumbukwe kuwa, karibu soda zote zimewekewa sukari kwa wingi sana na huenda kiwango cha sukari kilichopo kwenye soda kinazidi kiwango kinachostahili kuingia mwilini, hivyo sukari hii inapoingia mwilini inaulazimisha mwili kuhifadhi kiwango kikubwa cha maji kwenye mfumo wa chakula na mbaya zaidi unajiweka kwenye hatari zaidi ya kupata magonjwa ya kisukari.

Tafadhali zingatia kuwa, sio baadhi tu ya soda, bali soda karibu aina zote zinaweza kukuletea madhara haya.  Pia kukosa haja kubwa ni sababu nyingine inayochangia tumbo kujaa.  Ulaji vyakula ambavyo havina nyuzi lishe, na hata msongo wa mawazo ili kuweza kukabiliana nazo.


This post first appeared on Afya Na Kiasi, please read the originial post: here

Share the post

SABABU ZA KUJAA KWA TUMBO

×

Subscribe to Afya Na Kiasi

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×