Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

PILIPILI HUTIBU VIDONDA VYA TUMBO


Jitihada za kuutibu ugonjwa wa Vidonda Vya Tumbo zimeshachukua muda mrefu duniani na kwa bahati mbaya, uhakika wa tiba bado unaendelea kuwa kitendawili kisichoteguka hadi hii leo.

Hii ni kutokana na taarifa zinazozagaa kuwa vidonda Vya Tumbo ni aina ya magonjwa ya kibakteria tu na kwamba, dawa za antibiotic zinaweza kuutibu.

Kutokana na jambo hili ambalo limewafanya madaktari na wagonjwa wabaki na sintofahamu ya muafaka wa kudumu.

Mwanzoni mwa karne ya 20, Vidonda Vya tumbo viliaminika kuwa vilisababishwa na mgonjwa kuwa na “stress” zilizopitiliza pamoja na ulaji mbaya wa vyakula ambavyo vilisababisha ugonjwa huu.

Hivyo kwa kulijua hilo, matabibu walitoa tiba dawa, kuwapa mapumziko na kuwapa mpangilio maalumu wa chakula kisichoweza kuzalisha tindikali tumboni mwa mgonjwa na kuamini kuwa hiyo ingekuwa tiba tosha, lakini mafanikio yalibaki kuwa kitendawili.

Hakuna mtafiti aliyetulia tena toka hapo na hakika muda mfupi tu ikagundulika kuwa tindikali inayozalishwa tumboni kwa ajili ya umeng’enyaji wa chakula iitwayo ‘gastric acid’ndiyo iliyozalisha vidonda vya tumbo na hapohapo dawa zenye uwezo wa kuzuia tindikali hiyo isizalishwe tumboni mwa mgonjwa ikaanza kutolewa kwa mgonjwa.

Hii ilisaidia tu kupunguza idadi ya wagonjwa wa vidonda vya tumbo duniani kwani dawa hizo zijulikanazo kama ‘antiacids’ zilisaidia sana angalau kupunguza wagonjwa wa vidonda vya tumbo kulalamika kwa maumivu makali wanayoyapata.

Ilipofika mwaka 1982, madaktari bingwa kutoka Australia, Dk. Robin Warren na Dr. Barry Marshall walikuja na jibu la utafiti wao mpya kwamba kumbe kuna bakteria waitwao ‘Helicobacteria pylori’ ndio wanaosababisha ugonjwa wa vidonda vya tumbo na sio ulaji mbaya wa vyakula na stress.

Hata hivyo, habari hii ikaonekana kama inawachanganya matabibu kwa kuwa tayari walishatumia dawa za antibiotics kutibu na ikashindikana.

Hivyo mpaka hii leo madaktari na wagonjwa wengi bado hawataki kuaminishwa tena kwamba vidonda vya tumbo vinaweza kutibika kwa antibiotics na wengi hutumia dawa za mitishamba na tiba mbadala za aina tofauti zaidi kuliko kwenda hospitali kwa ushauri wa wataalam wa afya na dawa.

Bakteria hutokea wapi

Jibu la tafiti zangu binafsi linakuja kuwa stress humfanya mtu asile chakula sawasawa na hivyo tindikali ‘gastric acid’ hushambulia kuta za tumbo kwa ndani na kuzalisha vidonda vyenye bakteria hao.

Ila baadhi ya vidonda vya tumbo husababishwa na dawa kali anazotumia mgonjwa kujitibu maradhi fulani, halafu unywaji wa pombe bila kula na uvutaji wa sigara wa kupitiliza ni hatari sana!

Lakini ilipofika mwaka 1994, vyuo vya tafiti za magonjwa na dawa vingi tu duniani vilithibitisha kuwa utafiti wa madaktari toka Australia ulikuwa sahihi na kutoa mapendekezo kuwa wagonjwa waikubali tiba ya antibiotics kwa kuwa hata wao walifanya tafiti na kujiridhisha kuwa bakteria wa Helicobacter pylori walitibika kwa dawa hizo.

Mwaka mmoja baadae, rekodi zilionesha kuwa tayari asilimia 5 ya wagonjwa walishaanza kutumia antibiotics huku asilimia 75 ya wagonjwa walibaki wakitumia tiba mbadala bila imani na antibiotics.

Hii ilikuja kubainika katika utafiti uliofanyika baadaye kuwa asilimia 90 ya wagonjwa wa vidonda vya tumbo walikuwa bado hawajui kuwa ugonjwa huo husababishwa na bakteria wa Helicobacter pylori.

Hivyo, ilipofika 1996, Mamlaka za vyakula na dawa duniani zilitoa tamko rasmi juu ya matumizi ya aina maalum ya antibiotics kutibu vidonda vya tumbo, lakini mpaka sasa muelekeo unaonekana kuwa na mafanikio makubwa katika muda mfupi sana ujao.

Nani huugua

Vidonda vya tumbo ni ugonjwa unaoweza kumpata mtu yeyote lakini watu wenye makundi kama haya ndio waathirika zaidi.

Kundi la kwanza ni wale wote waliothirika kwa bakteria wa H.pylori, pia, watu wenye mazoea ya kumeza dawa za kutuliza maumivu mara kwa mara bila ushauri nao pia wako shakani.

Ila, kama katika ukoo wenu kuna historia ya wagonjwa wa aina hii, basi unaweza ukaupata pia, halafu wapo watu weye mazoea ya kunywa pombe kupita kiasi bila kula chakula cha kutosha nao wamo hatarini.

Ukiachana na hao, watu waliowahi kuugua magonjwa yenye uhusiano na mapafu, ini na figo pia huweza kuupata ugonjwa huu na kundi lingine ni watu wenye umri wa zaidi ya miaka 50, huweza pia kuupata ugonjwa huu japo sio wengi.

Dalili zake

Dalili za vidonda vya tumbo ziko nyingi lakini sio lazima zote mgonjwa azione ila baadhi ni lazima, nazo ni pamoja na kujisikia tumbo linaongezeka gesi, huwezi kunywa kiasi kikubwa cha vinywaji na hata maji pia, unapenda kukata kucha kwa meno mpaka unapatwa na vidonda vidoleni, ukila hukawii kujisikia njaa tena, ukiamka asubuhi unajisikia kichefuchefu, kujisikia mchovu nakujihisi kuumwa na kukosa hamu ya kula.

Ukiona dalili hizo unatakiwa ukamuone daktari haraka kwani ukichelewa kuidhibiti hali hiyo basi utajikuta ukitapika mara kwa mara na pengine matapishi yakawa na damu, au unaweza kupata kinyesi cheusi na chenye kunata na muathirika anaweza kujisaidia kinyesi chenye damu, hali ambayo inaonesha kuwa hali tumboni mwa mgonjwa sio shwari tena.

Nini cha kufanya?

Kwa kawaida, vidonda vya tumbo visivyo vikubwa hupona vyenyewe hasa kwa watu wenye kinga thabiti ya maradhi.  Hali hiyo haizuii kwa muathirika kwenda haraka hospitali kumuona daktari ambaye atachukua vipimo na kujua kitu gani kifanyike kwa ufasaha zaidi.

Lakini wakati unafanya hivyo, jaribu kunywa dawa za kupunguza tindikali tumboni ambazo hata daktari anaweza akakuandikia kwa kuwa tindikali ikizidi tumboni basi hata maumivu pia huzidi kwa mgonjwa na hata vidonda huzidi kutanuka.

Kitu kingine cha muhimu kufanya ni kuacha kutumia dawa zozote za kutuliza maumivu kama aspirini na Panadol au Ibrupfenol bila kushauriwa na daktari.

Usinywe maziwa

Watu wengi hushauri kunywa maziwa kwa kuwa hutuliza maumivu ya vidonda vya tumbo kwa kuziba kuta za ndani ya tumbo kwenye vidonda, lakini hiyo huwa kwa muda mfupi na hatimaye maziwa hayohayo yatachochea uzalishaji wa tindikali kwa wingi tumboni na kufanya vidonda visipone.

Kunywa juisi ya kabichi walau glasi moja kila siku.  Muombe daktari akuandikie multivitamin yenye vitamin D kwa wingi kwa kuwa ukitumia itasaidia kukausha vidonda kwa haraka.

Tumia pilipili

Pilipili ni dawa nzuri japo wapo wanaopinga hilo kwa madai kuwa itaongeza maumivu na kukuza vidonda, huo ni uongo!

Tafiti nyingi zilizofanyika duniani zinaonesha kuwa pilipili hufukuza bakteria katika vidonda na pia humuongezea mgonjwa madini ya chuma ambayo humfanya mgonjwa awe imara na apate nafuu haraka ila dawa za kutuliza maumivu zinahitajika unapotumia pilipili.

Kitalaamu, hakuna aina ya chakula ambacho kikiliwa huwa hakizalishi tindikali wakati wa kufyonzwa na kuta za tumbo hivyo kula vyakula vyenye tiba ndio kitu cha msingi na maana.


This post first appeared on Afya Na Kiasi, please read the originial post: here

Share the post

PILIPILI HUTIBU VIDONDA VYA TUMBO

×

Subscribe to Afya Na Kiasi

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×