Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

ZFA Wasema Watajiuzuru Kama Walitumiwa Maelezo Kuhusu Umri wa Wachezaji U-17



UONGOZI wa Chama cha Soka Zanzibar (ZFA), umesema, upo tayari kujiuzulu hata sasa iwapo kutagunduliwa kuwa walitumiwa maelekezo kuhusu Umri kwa wachezaji watakaoshiriki michuano ya Chalenji ya U-17.

Kauli hiyo ilitolewa na Makamu wa Rais wa ZFA Pemba, Ali Mohammed ambaye alikuwa meneja wa timu hiyo wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari huko Amaan jana.

Alisema, ZFA haina muongozo wowote uliotumwa kwao kuhusu umri au tarehe iliyotakiwa kwa ajili ya kwenda Burundi na kusema wapo tayari kutoa barua pepe zote mbili ikiwemo ya ZFA na Makamu wa Rais Unguja pamoja na namba za siri kwa wataalamu wa mitandao ili kuzikagua kwa kina kama kweli walitumiwa.

“Tumekuja hapa kusema kwamba ZFA haina ‘toleo’ lolote lililotumwa na CECAFA kwa ajili ya kuelezea umri au tarehe ya umri iliyotakiwa kwenda Burundi”.

“Tunatoa wito kwa wataalamu wa mitandao kuja ili tuwakabidhi ‘ barua pepe’zetu wazifanyie kazi kwa mujibu wa utaalamu wao, wakiliona hilo tupo tayari kuwajibika hata leo”, alisema.

Hata hivyo, alisema, pamoja na kwamba wameondolewa kuna hatua wanazozichukua kwa sababu hawajaridhika na sababu za kwenye barua za kuondolewa kwao.

“Karume Boys imeondoshwa na kuna hatua tunazichukuwa, moja ni kukata rufaa ambayo tumeianza juzi. Jambo la pili tumejiridhisha kwamba hatuna ‘toleo’ la aina yoyote inayotoa tafsiri ya U-17”, alieleza.

Alisema mashindano hayo yanaitwa U-17 na ndio kanuni za CECAFA zinavyosema katika kifungu cha nne, ambayo haina tafsiri ya U-17 ,lakini, kwa uzoefu wa ZFA tuliona watu wote ambao hawajafikia umri wa miaka 17.

“Ninachojua mimi na ZFA tafsiri yetu sahihi ilikuwa hii na mtakumbuka kwamba timu hiyo iliitwa kambini mwezi wa tatu na kulijitokeza wachezaji waliokuwa na umri mkubwa kabla ya timu hiyo kuvunjwa”.

“Baada ya kuundwa nyengine ambayo nayo watu waliiona ya kufungwa kutokana umri wa watoto ambao tumewapeleka, alisema.

Aidha, alisema, kabla ya kuipelekea timu hiyo walipokea barua pepe kutoka CECAFA ya kuwataka watume majina, paspoti namba na tarehe za kuzaliwa kwa wachezaji watakaoshiriki mashindano hayo kwa ajili ya kuthibitishwa.

Alisema, mnamo Aprili 7 mwaka huu, walituma majina hayo kwa kufuata maagizo na Aprili 11 saa 5:30 za usiku walitumiwa tiketi kwamba wameridhika na wao kama ZFA walifarijika na kusafiri kwenda Burundi.

Alisema, Zanzibar katika mashindano hayo walipangwa katika kituo cha Itega pamoja na Sudan, Ethiopia na Tanzania ambapo kwa bahati nzuri timu zote zilikutana katika uwanja wa Ndege na nchi ya mwanzo kuanza kulalamika ilikuwa Sudan ambayo ilisema katika timu zote ambazo zimetuma wachezaji wadogo ni Zanzibar pekee.

Lakini hatukwenda tu, CECAFA ilisema wachezaji wote ambao watakwenda ni lazima wawe wamefanyiwa kipimo cha MRI ambacho kitakuwa ni kithibitisho na kuchukuliwa Burundi, alisema.

Hata hivyo, alisema, hayo pia Nicolus Musonye hakuwatumia bali walipata maelekezo kutoka Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kupitia Alfred Kidau ambae alimpigia simu Makamu wa ZFA Unguja Mzee Zam Ali na kumuelekeza utaratibu uliopo kuhusu kipimo hicho.

Alisema mnamo tarehe 15 Aprili saa 9:30 za Burundi walikwenda katika mechi na wao ndio waliokuwa wa mwanzo kuikagua Sudan na kugundua kuna wachezaji wanne waliozidi umri na kuzuia pasi zao kabla ya nahodha wa Sudan naye kuwakagua na kuridhika na wachezaji wote.


This post first appeared on Maisha Yetu, please read the originial post: here

Share the post

ZFA Wasema Watajiuzuru Kama Walitumiwa Maelezo Kuhusu Umri wa Wachezaji U-17

×

Subscribe to Maisha Yetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×