Rais Dr.Magufuli Amesema hayo wakati wa maadhimisho ya miaka hamsini ya Benki kuu ya Tanzania na kusema kuwa hawezi kuendelea kuvumilia kuona wafanyakazi hewa wakiwepo na kwamba kasi ya kuwabaini inaenda sambamba na kutakiwa kurejeshwa kwa mishahara ambayo wamelipwa ama wanaendelea kulipwa.
Kuhusu Miaka Hamsini ya benki kuu, Rais Magufuli amesema benki hiyo inapaswa kujiimarisha katika kuyasimamia maduka ya kubadilisha fedha za kigeni ambayo baadhi yake hutumika kusafirisha fedha nje ya nchi kinyume na taratibu na kutakatisha fedha haramu zikiwemo zile zinatokana na mauzo ya dawa za kulevya sambamba na benki hiyo na hazina kuboresha ukusanyaji kodi katika madini.