Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Ajali Mbaya Yaua 6 na Kujeruhi 8, Same kilimanjaro

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

WATU sita wamefariki dunia na wengine nane wamejeruhiwa vibaya Katika ajali iliyohusisha basi dogo la abiria aina ya Hiace lililokuwa likitokea Mjini Same kuelekea Njoro wilayani Same, ambapo liligongana na gari ya mizigo aina ya Fuso muda mfupi baada ya kuondoka katika kituo cha abiria cha Same Mjini.

Daktari aliyezungumza na chanzo cha habari hii katika Hospital ya Wilaya ya Same, Dkt Mlay, amesema wamepokea maiti sita ambazo amebainisha kuwa wanaume ni watano na mwanamke ni mmoja.

Aidha, ameongeza kuwa Majeruhi nane walipatikana kufuatia Ajali Hiyo, ambapo katika Majeruhi hao nane wanawake ni wawili na wanaume sita na kati yao waliopewa rufaa kuelekea Hospitali ya KCMC -Moshi ni watatu, wanaume wawili na mwanamke mmoja.

Majeruhi Noel Bakari Kanumba, aliyekuwa anatokea Mjini Same kwenda Kavambughu, akizungumza na Mwandishi  katika wodi ya Wanaume katika Hospitali ya Same, amesema alikuwa amekaa kwenye Kiti Cha Mbele na dereva ambapo aligundua kuwa dereva yule alikuwa amelewa akamwonya asikimbize gari lakini hakutaka kumwelewa, ndipo gari lilimshinda na kuhama upande wake na kuelekea upande wa pili na kugonga Fuso upande wa dereva la Fuso hali iliyosababisha ajali ambapo dereva na abiria wake waliokuwa wamekaa kiti cha mbele walifariki dunia papo hapo.

Majeruhi wengine ni Musa Chikira (35), alikuwa anatokea Mjini Same kwenda Njoro na Mariam Omary Mbaga aliyekuwa katika wodi ya wanawake.
Majerhi wa ajali hiyo, Noel Bakari Kanumba (36), alikuwa anatokea Same Mjini akienda Kavambughu.
Majeruhi wa ajali hiyo, Musa Chikira (35), akiwa Amelazwa Katika Wodi ya wanaume, hospital ya Wilaya ya Same.
Majeruhi wa ajali hiyo, Musa Chikira (35), Akiwa Amelazwa Katika wodi ya wanaume, hospital ya Wilaya ya Same.


This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

Ajali Mbaya Yaua 6 na Kujeruhi 8, Same kilimanjaro

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×