Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

MPYA:TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. KUKANUSHA TAARIFA KUHUSU TANGAZO LA AJIRA SERIKALINI

 

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI.


KUKANUSHA TAARIFA KUHUSU TANGAZO LA AJIRA SERIKALINI

Kuna tangazo ambalo linasambazwa kupitia baadhi ya mitandao ya kijamii lenye kichwa cha habari ‘’Sekretarieti ya Ajira yatangaza zaidi ya nafasi za kazi 1,000’’. Likionyesha kuwa Serikali kupitia Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma inawatangazia watanzania wenye sifa na uwezo kujaza jumla ya nafasi wazi za kazi 1,101 kwa niaba ya waajiri mbalimbali Serikalini.
Katibu wa Sekretarieti ya Ajira anapenda kuwataafu wadau na wananchi wote kwa ujumla kuwa taarifa hiyo haina ukweli wowote na inalenga kuupotosha Umma, hivyo wananchi wote wanapaswa kuzipuuza. Matangazo yote ambayo hutolewa na Serikali kupitia Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma ni lazima yaonekane kwenye Tovuti ya Sekretarieti ya Ajira www.ajira.go.tz au portal ya Ajira ambayo ni portal.ajira.go.tz.
Kama mnavyofahamu hivi karibuni Serikali ilitoa taarifa ya kusitisha ajira mpya serikalini kwa ajili ya zoezi la uhakiki wa Watumishi hewa kama ambavyo taarifa ilivyotolewa hapo awali, kwa kuwa zoezi hilo bado halijakamilika tunaomba wananchi wote na wadau wa Sekretarieti ya Ajira waendelee kuvuta subira hadi pale zoezi hilo litakapokamilika na taarifa rasmi itatolewa na Mamlaka husika.
Sekretarieti ya Ajira inapenda kuomba radhi kwa wale wote waliopata usumbufu kutokana na tangazo hilo lenye nia ya kupotosha Umma.
Aidha,tunaendelea kuwasisitiza wadau wetu wote kuwa, wanapoona matangazo ya kazi yanayodaiwa kutolewa na Sekretarieti ya Ajira katika baadhi ya mitandao ya kijamii wasiyokuwa na uhakika nayo wajiridhishe kwa kuangalia katika tovuti na portal ya Sekretarieti ya Ajira kabla ya kuyafanyia kazi.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma. Simu: 0687624975
30 Septemba, 2016.


This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

MPYA:TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. KUKANUSHA TAARIFA KUHUSU TANGAZO LA AJIRA SERIKALINI

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×