Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Rais Magufuli: Tutafungua Shule za Msingi, Sekondari na Chekekea Hivi Karibuni, Corona Imepungua Sana

Rais wa Tanzania, Dr John Magufuli Amesema atafungua shule za msingi na sekondari hivi karibuni, kama ataridhishwa na kasi ya upunguaji wa maambukizi ya ugonjwa wa Corona

Rais Magufuli amesema hayo leo Ijumaa tarehe 5 Juni 2020, wakati akifungua mkutano mkuu wa uchaguzi wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), jijini Dodoma.

Amesema, maambukizi ya corona yamekuwa yakipungua siku hadi siku huku akiendelea kuwasisitiza wananchi kuchukua tahadhari  ya ugonjwa huo.

Huku akishangiliwa na umati wa mkutano huo,  Rais Magufuli amefurahishwa na washiriki wa mkutano huo walioujaza uwanja wa Jamhuri, Dodoma kutokuvaa barakoa huku akionyesha kushangazwa na Spika wa Bunge, Job Ndugai kuvaa barakoa akiwa ndani ya Bunge. 

“Corona imekwisha Ndiyo Maana hata mabarakoa hakuna, hata leo tunaonana tu hapa kawaida, ndiyo maana nilikuwa namshangaa Spika Ndugai akiwa Bungeni yupo kiti chake peke yake lakini amelivaa hilo libarakoa mdomoni, Watanzania tumtangulize Mungu."-Amesema




This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

Rais Magufuli: Tutafungua Shule za Msingi, Sekondari na Chekekea Hivi Karibuni, Corona Imepungua Sana

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×