Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Picha : MBUNGE AZZA HILAL ACHANGIA MIL. 4.8 KWA AJILI YA UPAUAJI WA JENGO LA AKINA MAMA ZAHANATI YA ZUNZULI

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Shinyanga Mhe. Azza Hilal Hamad (CCM) amechangia shilingi 5,895,000/= kwa ajili ya upauaji wa jengo la wodi ya akina mama katika zahanati ya kijiji cha Zunzuli kata ya Mwenge halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika leo Ijumaa Juni 7,2019 katika kijiji cha Zunzuli,kilichohudhuriwa pia na Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Mhe.Jasinta Mboneko,mbunge huyo alisema fedha hizo zitatumika kununua mbao na mabati kwa ajili ya ujenzi wa wodi ya akina mama.

“Baada ya kuona zahanati hii ya Zunzuli haina wodi ya akina mama,nilichokifanya ni kutafuta fedha kwa ajili ya upauaji,namshukuru Mungu wadau wangu wamenishika mkono,nimepata kiasi cha shilingi milioni 4.8 kwa ajili ya kununua mbao na mabati ili wodi hii ya wazazi ambayo wananchi wameijenga hadi kwenye renta ili iweze kupauliwa”,alisema Azza.

“Zahanati hii ya Zunzuli iliyojengwa mwaka 1994 ina chumba kidogo tu chenye vitanda viwili, akina mama wanapokuwa wengi huduma inakuwa tatizo,takwimu zinaonesha zahanati hii inapokea akina mama wanaojifungua kati ya 20 hadi 25 kwa mwezi ndiyo maana nikaona umuhimu wa kuwatafutia fedha za upauaji ili akina mama waweze kupata huduma wanayostahili”,aliongeza mbunge Azza.

Alisema jukumu lake kubwa kama mbunge wa viti maalum na mbunge mwanamke ni kuhakikisha huduma za afya zinaboreshwa na hiyoni kuunga mkono kwa vitendo jitihada zinazofanywa na Rais wa awamu ya tano Dkt. John Pombe Magufuli katika kuboresha sekta ya afya.

Kwa upande wake,Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Mhe. Jasinta Mboneko aliwataka wananchi kutumia fedha zilizotolewa na mbunge kwa malengo yaliyokusudiwa na kuwakumbusha kuwa mstari wa mbele kuchangia shughuli za maendeleo badala ya kusubiri serikali pekee iwaletee maendeleo.

Mboneko pia aliwahamasisha wanawake kuhudhuria kliniki na kujifungulia kwenye vituo vya afya huku akiwasisitiza akina baba kutunza na kukaa vizuri na wake zao badala ya kuwanyanyasa na kupeleka watoto shule badala ya kuwaozesha.
ANGALIA PICHA HAPA CHINI


Wa pili kulia ni diwani wa kata ya Mwenge Edward Maganga akimwongoza Mbunge wa viti Maalum Mkoa wa Shinyanga Mhe. Azza Hilal Hamad (wa pili kushoto) na Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Mhe.Jasinta Mboneko (katikati) walipowasili katika zahanati ya Zunzuli leo Juni 7,2019 . Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Muonekano wa jengo la wodi ya akina mama katika zahanati ya Zunzuli kata ya Mwenge ambapo limefikia kwenye renta na tayari Mbunge amepata fedha kwa ajili ya upauaji.
Mganga mfawidhi Zahanati ya Zunzuli Dkt. Manumi Julius akionesha jengo la zahanati ya Zunzuli.
Mbunge wa viti Maalum Mkoa wa Shinyanga Mhe. Azza Hilal Hamad (CCM) akizungumza na wananchi wa kijiji cha Zunzuli na kuwaambia amepata fedha kwa ajili ya upauaji wa jengo la zahanati ya akina mama zinawekwa kwenye akaunti ya kijiji.
Mbunge wa viti Maalum Mkoa wa Shinyanga Mhe. Azza Hilal Hamad akizungumza kwenye mkutano wa hadhara katika kijiji cha Zunzuli.
Wananchi wakiwa kwenye mkutano huo.
Mbunge wa viti Maalum Mkoa wa Shinyanga Mhe. Azza Hilal Hamad akizungumza kwenye mkutano wa hadhara katika kijiji cha Zunzuli.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Mhe.Jasinta Mboneko akizungumza katika mkutano wa hadhara katika kijiji cha Zunzuli na kuwahamasisha wananchi kuendelea kujitokeza kushiriki katika shughuli za maendeleo.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Mhe. Jasinta Mboneko akizungumza na wananchi wa kijiji cha Zunzuli.
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga,Mhe. Hoja Mahiba akizungumza kwenye mkutano huo.
Afisa Mtendaji wa kata ya Mwenge,Gabaruda Gidawadini Gidaweda akizungumza katika mkutano huo.
Mbunge wa viti Maalum Mkoa wa Shinyanga Mhe. Azza Hilal Hamad (CCM),Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Mhe. Jasinta Mboneko  na Diwani wa kata ya Mwenge, Mhe. Edward Maganga wakifurahia jambo kwenye mkutano wa hadhara kijiji cha Zunzuli.
Viongozi mbalimbali wa CCM wakiwa kwenye mkutano huo.
Diwani wa kata ya Mwenge, Mhe. Edward Maganga akizungumza katika mkutano huo.



Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Mhe. Jasinta Mboneko akifurahia jambo wakati akiagana na wakazi wa kijiji cha Zunzuli kata ya Mwenge halmashauri ya wilaya ya Shinyanga baada ya kufanya mkutano wa hadhara.

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog


This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

Picha : MBUNGE AZZA HILAL ACHANGIA MIL. 4.8 KWA AJILI YA UPAUAJI WA JENGO LA AKINA MAMA ZAHANATI YA ZUNZULI

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×