Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

URUSI KUZIMA MTANDAO WA INTANETI KUJILINDA NA MAADUI

Urusi chini ya Rais Vladimir Putin imekuwa ikilaumiwa vikali na Nchi wanachama wa Nato kwa mashambulizi ya kimtandao.

Urusi inajipanga Kuzima Mtandao wa intaneti kwa muda, na hivyo kujitoa kwenye mawasiliano na dunia kama sehemu ya majaribio yake ya kujikinga dhidi ya mashambulio ya kimtandao.

Zoezi hilo litafanya mawasiliano baina ya raia na mashirika ya Urusi kubaki ndani ya nchi badala ya ya kupitia njia za kawaida za kimtandao kimataifa.

Rasimu ya sheria ya kuruhusu mabadiliko ya kiufundi ili kuiwezesha nchi hiyo kuendesha mtandao wake wenyewe iliwasilishwa bungeni mwaka jana.

Jaribio hilo linatarajiwa kufanyika kabla ya tarehe mosi Aprili, lakini siku rasmi ya kuzimwa mtandao haijatajwa.


Rasimu hiyo ya sheria, iliyopewa jina la Programu ya Taifa ya Uchumi wa Kidijiti, inawataka watoa huduma za intaneti nchini Urusi kuwa na uwezo wa kuendelea na huduma zao hata pale ikitokea nchi za kigeni zikiamua kuitenga Urusi.

Nchi wanachama wa Nato na washirika wake wamekuwa wakitishia kuiwekea vikwazo vya kimtandao Urusi ambayo wanaituhumu kwa kufanya mashambulio ya kimtandao.

Njia mojawapo inayopangwa na Urusi katika kujilinda huko ni kutengeneza mfumo wake binafsi wa anuani za kimtandao ufahamikao kama DNS, waweze kupata mawasiliano hata pale watakapotengwa ama kujitenga.

Chanzo:Bbc


This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

URUSI KUZIMA MTANDAO WA INTANETI KUJILINDA NA MAADUI

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×