Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

VIDEO: Prof. NDALICHAKO AKITOA UFAFANUZI KUHUSU TANGAZO LA AJIRA ZA WALIMU LILILOTEWA IVI KARIBUNI - Majibu ya serikali kuhusu wanaosubiri ajira za ualimu

 
December 15 2016 Waziri wa elimu, sayansi na teknolojia Prof. Joyce Ndalichako alikutana Dodoma na wadau mbalimbali wa sekta ya elimu ili kujadili namna sahihi ya kuboresha sekta hiyo katika kipindi cha awamu ya tano ambapo katika baadhi ya vitu alivyogusia ni pamoja na suala la ajira kwa walimu.
Waziri Ndalichako amesema…>>>’Utaratibu wa kuajiri tunauboresha, zamani ilikuwa ukisoma ualimu unapangiwa sehemu ya kazi bila hata kuhakikiwa lakini sasa ni lazima kila anayemaliza mafunzo ahakikiwe kwanza ndipo hatua zingine zinafuatwa‘ –Pro. Joyce Ndalichako
Tumebaini kwamba serikali imekuwa ikipoteza fedha nyingi kwa kuajiri watu wasiokuwa na sifa, tayari katibu mkuu wa wizara yangu ameshatoa tangazo kwa wahitimu wote waliomaliza mafunzo ya sayansi mwaka 2015 wawasilishe vyeti vyao ili vihakikiwe‘ –Pro. Joyce Ndalichako
Na wale watakaoonekana wana vyeti visivyokuwa na mashaka ndio watakaopata nafasi kwahiyo zoezi la ajira kwa walimu limeanza hivyo tunaamini tatizo la ajira kwa walimu haliakwisha lakini tutakuwa tumelipunguza kwa nafasi kubwa‘ –Pro. Joyce Ndalichako

unaweza kuendelea kumsikiliza Pro. Joyce Ndalichako kwenye hii video hapa chini…
 
BAADA ya kusitisha ajira za umma kwa takribani miezi tisa, hatimaye serikali imetangaza ajira kwa wahitimu wa ualimu kwa shule za sekondari.
Hata hivyo, ajira mpya zilizotangazwa na serikali jana, zinawahusu walimu wa ngazi ya stashahada na shahada ya ualimu wa masomo ya sayansi na Hisabati Kwa Shule za sekondari.
Kwa mujibu wa tangazo lililotolewa jana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Maimuna Tarish, na kuchapishwa kwenye tovuti rasmi ya wizara hiyo, serikali inatarajia kuajiri walimu wa masomo ya sayansi na hisabati kwa shule za sekondari waliohitimu mwaka jana.
Hata hivyo, idadi ya walimu wanaohitajika kwa ajili ya kufundisha masomo hayo haikuelezwa katika tangazo hilo. "Ajira hii ni kwa walimu wa stashahada na shahada za mafunzo ya ualimu wa masomo ya hisabati na sayansi waliohitimu mwaka 2015.
Wahitimu hao wanatakiwa kuwasilisha nakala za vyeti vyao vya elimu ya sekondari (kidato cha nne na sita) na taaluma ya ualimu (stashahada na shahada) kwa ajili ya uhakiki.
"Nakala hizo ziwasilishwe kupitia barua pepe ya wizara [email protected] kuanzia tarehe ya tangazo hili (jana) hadi Ijumaa Desemba 16, 2016.
Yeyote ambaye vyeti vyake havitahakikiwa, hatafikiriwa katika ajira," tangazo hilo lilieleza. Katika mwaka huu wa fedha, serikali imepanga kuajiri watumishi 71,496 kwenye sekta mbalimbali zikiwamo elimu, afya na viwanda.
 


This post first appeared on MASWAYETU, please read the originial post: here

Share the post

VIDEO: Prof. NDALICHAKO AKITOA UFAFANUZI KUHUSU TANGAZO LA AJIRA ZA WALIMU LILILOTEWA IVI KARIBUNI - Majibu ya serikali kuhusu wanaosubiri ajira za ualimu

×

Subscribe to Maswayetu

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×