Get Even More Visitors To Your Blog, Upgrade To A Business Listing >>

Waziri wa habari utamaduni na michezo atuma salamu za pole shirikisho la riadha!

Dar es Salaam. Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye ametoa salamu za Pole kwa Rais wa Shirikisho la  Riadha  nchini, Anthony Mtaka kufuatia kifo cha mshiriki kutoka nchini Kenya, Charles Rioba (36) aliyefariki katika mashindano ya Kilimanjaro Marathon yaliyofanyika Februari, 26 mkoani Kilimanjaro.
Rioba alishiriki kwa hiari mbio zijulikanazo kama ‘run for fun’ za Kilometa 21, zilizohusisha wananchi mbalimbali wakiwemo pia viongozi wastaafu.
Lakini akiwa katika mbio hizo alianguka na kupatiwa huduma ya kwanza kisha kupelekwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Kilimanjaro Christian Medical Centre (KCMC) na baadae kufariki dunia.
Waziri Nape ametoa pole pia kwa waandaaji wa mashindano hayo na wote ambao wameguswa na msiba huo



This post first appeared on HABARI ZA SIASA NA MUZIKI, please read the originial post: here

Share the post

Waziri wa habari utamaduni na michezo atuma salamu za pole shirikisho la riadha!

×

Subscribe to Habari Za Siasa Na Muziki

Get updates delivered right to your inbox!

Thank you for your subscription

×