Magufuli Ampangia Kazi Nyingine Kamishana wa TRA...!!! Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, jana tarehe 23 Machi, 2017 amemteua Bw. Alphayo Kidata kuwa Katibu Mkuu, Ikulu. Bw. Alphayo Kidata anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Peter Ilomo ambaye amestaafu.